NIACHE NILIE ---4 😓😓😓😓

7 days ago

Tulifika na kuwakuta watumishi wake na walituambia saa hizi kwali mtumishi hamtaweza kumuona labda mje kesho au tuachie namba zenu za simu. Baba aliwapa na hivyo tulirudi nyumbani bila kupata huduma yoyote. 

Hali yanguilizidi kubadilika kila siku maajabu ya kila aina yakiendelea kuonekana kwenye mwili wangu. Niliendelea kukaa nyumbani huku nikiendelea kuombewa na kila mtu. Mungu alishusha huruma zake na hali yangu ikaanza kuwa nzuri shuleni niliitwa ofisini na mazungumzo yalikuwa hivi.



Mwalimu : Emiliana kuna mzazi wako ameleta madaftari hapa na amesema tukukabidhi na hayo mengine usiyatumie.

Emiliana : Mwalimu mzazi yupi huyo?

Mwalimu : Kwa taarifa alitokea hapa amesema ni baba yako

Emiliana : Mwalimu kwa nin amesema haya mengine nisiyatumie kwani yana nini?

Mwalimu: Sielewi

Niliachana na mwalimu na kuelekea darasani, kichwani mwangu nikielewa aliyeleta hayo madaftari na kusema ni baba yangu atakuwa ni baba yangu mzazi. 

Nilipotoka shuleni nilifika nyumbani na kuwaelezea wazazi wang hali halisi na waliendelea kulifuatilia mwenyewe. Niliendelea kwenda shuleni vizuri lakini siku moja nikiwa naelekea shuleni nilipanda gari vizuri na nilipofika kituoni nilishuka na wakati naelekea na njia ya kwenda shule alitokea, mwanamke mmoja akiwa amevaa kininja alinipiga ngumi ya mgongo na damu ziliruka mdomoni, mwangu na nilipoanza kuomba msaada kwa watu waliokuwa wakipita walinisaidia na niliweza kuwaonyesha muhusika aliyenipiga lakini walidai hawamuoni. 

Sikwenda tena shuleni ilibidi nirudi nyumbani. Nilirudi nyumbani hali ikizidi kuwa mbaya zaidi na niliendelea kutapika damu tu. Niliendelea kukaa nyumbani kwa huduma zaidi, niliendelea kuombewa hadi hali ilipojirudi katika hali yake. Mungu alinisadia na niliendelea tena kwenda shule kama kuwaida. 

Na safari ya mama yangu ya kutoka Mbeya na kurudi Arusha ilifika na alirudi salama na kuendelea kunipa huduma. Niliendelea kwenda shule vizuri bila tatizo,lolote lile. 

Baada ya muda tena nikiwa natoka shule nilikutana na vijana watatu wakiwa wamevaa kininja na walikuwa katika kituo cha kupanda gari. Nilifika na nilikuwa nasubiria usafiri na hao walikuwa na tax nyesi isiyokuwa na namba yoyote, walinifuata na kuniambia haya.

Wao Wewe unaitwa Emiliana

Mimi: Hapana mimi siitwi Emiliana

Wao: Wewe ni Emiliana kwani baba yako si anaitwa Ernest?

Mimi: Siitwi Emiliana jamani na sina baba anayeitwa Ernest?

Walichukuwa uwamuzi wakuninyang’anya madaftari yangu mawili na biki yangu moja. Na walipochukua yale madaftari na kusoma jina waliniambia hivi 

“Tumekuuliza unaitwa Emiliana ukakataa mbona hapa umeandika Emiliana?” Sikujibu chochote zaidi nilizidi kulia uku nikiendelea kuomba msaada kwa watu waliokuwa kituoni hapa na kila niliyemuomba msaada alikuwa akicheka na kusema malaria imenipanda kichwani ingawa nilijaribu kuwaonyesha wale vijana lakini walidai hawamuoni mtu yeyote Yule aliyekuwa akiniletea vurugu na kuzidi kuniambia niende hospitali labda malaria imenipanda kichwani. 

Nililia sana ingawa sikupata msaada kwa wale watu wote waliokuwa katika eneo lile. Vijana wale waliamua kunitemea mate kwenye banda la uso na walipomaliza waliondoka na walienda na yale madaftari yangu na ile kalamu yangu, kichwa kilianza kuniuma paleplae na alitokea kijana mmoja ambae ni kondakta wa magari yakuelekea nyumbani akanishika mkono na kuniiingiza kwenye gari nakuelekea nyumbani. 

Nilifika nyumbani salama huku nikiwa na maumivu makali sana kichwani, nilimuelezea mama yangu hali halisi iliyonikuta na akaniombea niijipumzisha hali ikiendelea kuwa mbaya. 

Usiku uliingia maumivu yakiendelea kuwa makali zaidi, kichwa kiiendelea kuuma sana haswa kwa panda la uzo, ndipo damu zilizidi kutoka utosini na nilipozidi kulia yalitoka macho toka utosini na nilipozidi kulia yalitoka machozi ya damu hali ilizidi kuwa mbaya kiafya.



Mama aliendelea kuniombea bila kukata tamaa niliendelea kutiwa moyo na watumishi mbalimbali na rafiki zangu maombi yaliendelea kila sehemu waliokuwa Mbeya ambao ni ndugu wa mama yangu mzazi waliendelea kuniombea, waliokuwa Moshi waliendelea na maombi na hata kwa ndugu wa mama walioko Iringa walindelea na maombi na kwa watumishi wote walioko Arusha waliendelea na maombi bila kukata tamaa, hali ilizidi kuwa mbaya kwa upande wangu. Ilifika mahali mama yangu alikata tamaa nakusema haya.

Ruth Ee Mungu kama ni mtoto ni wewe ulinipa, na nimemlea hadi umri huu wa miaka 18, kama ni mapenzi yako naomba yatimizwe. Na kama si yako naomba uzima kwa mtoto wangu.

Aliyaongea kwa uchungu na kwa machozi ya uchungu. Ndugu na waumini wenzake wakiendelea kumtia moyo kwa wakati mgumu uliomfika. 

Na wengineo, walijua ni lazima nife tu chakushangaza baadhi ya wengineo waliokuwa ni majirani wa mama yangu walizungumza maneno machafu mtaani bila kuwa na huruma.

Waliongea haya:

- Inawezekana mama yake anaficha siri yamwanae, uenda katoa mimba sasa ndiyo hayo.

- Wengine wakasema haya uenda mama yake mwenyewe anamuuwa mwanae kila mmoja alitamka analoweza kutamka na kwa walio mzarau Mungu walisema Mtu gani huyu ambae anaombewa na watu wote hao lakini haponi alafu eti ni walokole, walokole si wanasemaga, wanaponya mbona huyo haponi ni maneno yaliyoendelea kutolewa na binadamu ambao hawakuwa na hofu ya Mungu ndani yao Nilizidi kuumia zaidi kwa maneno makali na yasiyokuwa na uzima ndani yake.

BONYEZA MAANDISHI HAYA KUPATA MEMES BUREE

ITAENDELEA 

Post a Comment

Previous Post Next Post