GEORGE; NATAMANI NIFE LAKINI BADO SIJAITWA BABA 07

“Mmenipangia, hii ilikua ni mipango yenu kabisa ili kuja kunidhalilisha! Yaani umekaa na kimwanamke chako huko unakuja hapa kusema nimebaka!” Nilijikuta naanza kupiga kelele, kwa akili yangu niliamini kabisa kuwa Jack alikua amepanga na yule binti. Tofauti na nilivyodhani labda Jack atanigeuzia kibao haikua hivyo, alimshika yule binti mkono na kutoka naye nnje, sijui waliongea nini lakini mimi hakuniongelesha kitu chochote, ni kama alinidharau.

Nilitoka ofisini kwa aibu na kwenda nyumbani, nilikua na hasira sana na hasira zangu zote zilikua ni kwa wanawake, siku hisikulala kabisa hata kesho yake si kwenda kazini nahata sikujali chochote. Kesho yake mchana wakati naangalia kwenye mitandao ya kijamii nikaona tangazo la Massage (kukandwa), sijui kwanini lakini niliamua kwenda.

Ilikua ni mara yangu ya kwanza kufanyiwa hivyo na niliamini kuwa kama nikifanya hivyo basi nitakua vizuri. Kweli yule dada alinifanyia vizuri baada ya kumaliza aliniuliza.
“Utaweza kujisugua mwenyewe au nikusaidie….” Nilikua naenda kuoga na wakati huo nilikua nimefunga kitaulo tu kiunoni, nilishangaa kwanini ananiuliza hivyo.
“Inamaana unataka kuniogesha?” Nilimuuliza.
“Ndiyo, hakuna shida au unaona aibu?” Nilibaki kimya bila kuongea kitu chochote, nilimuangalia kwa matamanio nikavua kile kitaulo na kumuacha aniongeshe.
“Kuna huduma nyingine unataka?” Aliniulzia,
nilikua simuelewi lakini namna alivyokua anaongea ananishikashika niligundua anataka nini.

“Kama ipo sawa bei gani?” Nilimuuluiza.
“Una elfu hamisini?”
“Ndiyo, lakini sitaki kufanya hapa, sitajisikia vizuri kama upo tayari nikitoka hapa tukutane sehemu.” Nilimuambia, hata hakubisha, hata hakujali kama yuko kazini, nilitoka pale tukaondoka naye, nikamchukua mpaka nyumbani kwangu, mwanzo alisita lakini nilimbembeleza mpaka akingia.

Tukaingia kwenye kufanya mapenzi nilijikuta tu napata hasira, baada ya kumaliza nikaanza kumuingilia kinyume na maumbile, mimi nilidhani kama namkomoa lakini yeye alikua kazoea na aliona sawa.
“Utaongeza pesa!” Aliniambia, nilijikuta nashangaa, ingawa nilikua na pesa ya kumpa lakini nilikataa, aligoma kufanya mapenzi kinyume na maumbile bila mimi kumuongezea pesa, palepale nilimvamia na kuanza kumpiga, nilimpiga sana mpaka kuvuja damu kisha nikamuingilia kinyume na maumbile na kumfukuza kwangu.

Alipoondoka nilijisikia raha sana.
“Hii ndiyo dawa ya hawa Malaya, hakuna wa kunisumbua tena, yaani akileta ujinga ni kupiga wanawake wote ni washenzi!” Nilijiongelesha wakati anaondoka, ingawa kuna kitu kilinifanya kujisikia vibaya lakini kuna namna nilifurahia kitu nilichokifanya, kuna namna nilikua najisikia vizuri na kuona kuwa yalikua ni makosa ya wanawake na sio mimi.

Baada ya hapo hiyo ndiyo ilikua kazi yangu, kununua wanawake nawalazimisha kufanya mapenzi kinyume na maumbile wakiakataa nawapiga. Wakati mwingine hata mwanamke akikubali nilikua nampiga, kwangu ilikua ni kama kufanya mapenzi mwenyewe, kumnyanyasa mwanamke na kumdhalilisha ilinipa raha ya ajabu kuliko tendo la ndoa lenyewe. Nilibadilisha wanawake kama nguo na hata siku moja sikujali hisia zao. Kwangu mimi niliona kama ni kitu cha kawaida. Baada ya kuona kuwa mtaani najulikana na karibu kila mwanamke nilihamia Facebook.

Huko ndipo ilikua ni rahisi kwangu kupata wanawake, nilikua naingia naangalia mdada mzuri kisha namtongoza, akiniomba pesa namtumia na kujifanya kama nimetoka kuumizwa na sasa hivi nataka mwanamke wa kuoa. Ilikua ni njia nzuri sana kwangu kwani muda wote nilikua online, wakiniomba pesa nawatumia ili tu waniamini na wao nawaomba picha za uchi wananitumia.

Baada ya hapo tunapanga kuonana na nikikutana nao nakua nataka kufanya nao mapenzi kinyume na maumbile. Kwakua wapo kwangu wanakua hawana namna, nilikua nadili sana na wanafunzi wa chuo ambao ndiyo hupenda kuomba pesa na kuamini kirahisi. Hiyo tabia iliendelea ikawa ndiyo maisha yangu, nikawa mtu wa kutuma nauli, pesa zangu zote ziliishia kwenye wanawake wa mitandaoni, nilikua nakaa mpaka saa nane usiku nachart na wanawake zaidi ya mia mbili kwenye simu kila mmoja akiamini kuwa nampenda na nitamuoa.

Nilizoea hiyo hali kiasi kwamba hata mahusiano ya kawaida kwangu ilikua ngumu, nilikua sina mwanamke zaidi ya wanawake wa kwenye mitandao na kila wiki nilikua nakutana na wanawake wawili wapya, nikishatembea naye nilikua sirudii kabisa, nikikutana naye kimwili nahakikisha namfanyia kitu cha ajabu ili asirudi kwangu tena. Walikua hawawezi hata kunishitaki kwani wengi wao wanakua washanitumia mapicha ya uchi hivyo nawaambia kabisa kama ukimuambia mtu yeyote basi nitazivujisha.

Nilibadilika sana, nikawa ni mtu wa kukaa nyumbani, sina mahusiano yoyote, ndugu zangu wakiniuliza kuhusu kuoa naishia kuwapiga kalenda, walinisumbua sana huku dada zangu wakinitafutia wanawake lakini nawakataa. Nakumbuka kuna wakati Dada yangu aliniunganisha kwa mtoto wa rafiki yake, alikua ni mzuri sana binti wa miaka 23 ndiyo kamaliza chuo, nilikua simtaki kwani nilikua sina haja naye lakini Dada alinisisitiza sana hata kuonana naye.

“Muone tu kwanza utaamua mwenyewe!” Aliniambia, kwakua ni mtu nilikua namheshimu nikawa sina namna, nilikubali kukutana na yule binti kuongea. Siku ya kwanza kumuona tu nilihisi kuchanganyikiwa, yule mtoto alikua ni mzuri, alikua kaumbika na alikua na nidhamu sana.
“Huyu nitamuoa, najua nikimuoa huyu wale Malaya wote walionipotezea muda watakuja kwangu kunipigia magoti!” Alinivutia sana lakini huwezi amini kila nikimuangalia nilikua nawaza kulipa kisasi, nilikua naamini kama ulimwengu mzima ulikua umenikosea hivyo natakiwa kuwalipia kisasi na nilijua kama nikimuoa huyo binti basi wote wataumia.

Siku hiyo nilikua tofauti kabisa niliongea na huyuo binti mambo mengi, nilimuambia kuhusu mimi kuwa nilishaingia kwenye mahusiano yakaniumiza hivyo nilikua nataka mtu siriasi na si mtu wa kunichezea, aliniambia kuwa yeye hajawahi kuingia kwenye mahusiano kwani katoka kwenye familia ya kilokole hivyo amejitunza kwaajili ya mume wake, aliniambia kabisa kuwa hawezi kukutana na mimi kimwili mpaka pale ambapo tutaingia kwenye ndoa.

Nilimuambia sawa hata mimi nataka hivyo basi tuliongea mengi na huo ndiyo ukawa mwanzo wa mahusiano yetu. Wazazi wake walikua wananijua lakini baada ya kama miezi miwili hivi ya kujuana ndipo alinitambulisha kwao rasmi kama Mchumba wake. Nilifurahi sana kutambulishwa, nilijisikia kama mtu na kweli yule binti alinifanya nijihisi nina furaha. Alikua anakuja kwangu, anakua huru kunipikia na mambo mengine kasoro kufanya tendo la ndoa tu.

Pamoja na kuwa naye lakini sikuweza kuacha mambo yangu, bado nilikua nabadilisha wanawake kama nguo na nilikua bize kwenye mitandao. Simu yangu ilikua na Password kama mia hivi kwani sikutaka ajue chochote kuhusu mimi. Siku moja akiwa kwangu sijui kilitokea nini wakati nachart nikawake simu chini nikatoka kidogo, kurudi namkuta kashikilia simu yangu anaangalia meseji zangu, huwa sifuti kitu chochote hivyo aliona kila kitu.

Nilimuangalia alivyobadilika, alikua mwekundu machozi yanamtoka kama maji, nilipiga magoti kumbembeleza sana nikamuambia sio kama hao wanawake naonana nao lakini ni kwakua tu nilishazoe kipindi siko naye, nilimuomba msamaha na kumuambia kuwa nitaacha lakini hakua tayari kunisikiliza, aliondoka bila kuaga na kuniacha nikiwa sina chakufanya.

Baada ya kuondoka nilimuomba sana msamaha, wiki mbili nilikua namuomba msamaha, naomba hata turidiane naye lakini hakua tayari, kama unavyojua wanawake baada ya kuona nazidisha kuomba msamaha alilainika na kunisamehe. Nilitaka kuharakisha mambo ya ndoa lakini yeye hakutaka, aliniambia anataka kunichunguza kwanza kama nimebadilika au la, kauli hiuyo iliniumiza na kuona kama anataka kuniacha kwani huko mwanzo yeye ndiyo alikua analazimishia sana mambo ya ndoa.

Siku moja alikuja kwangu kunisalimia, alitaka kushika simu yangu lakini nilimkatalia. Alikasirika na kuanza kunitukana huku akitaka kuondoka. Nilimshika na kumvuta kitandani huku nikimpiga makofi.
“Hivi unajiona nani wewe mbwa? Unajiona nani nakuambia? Nakuuliza unajiona nani? Kwanza mtu mwenyewe sikukutongoza ni Mama yako tu amekuuza kwangu halafu unajifanya mjanja! Niliongea huku nikimshika na kumvua nguo kutaka kufanya naye mapenzi, nilimuambia hata akipiga kelele kila mtu anajua ni mpenzi wangu na haitasaidia. Nilimbania chini huku nikijaribu kufanya naye mapenzi lakini huwezi amini nilishindwa kufanya naye mapenzi kabisa.

Uume wangu ulikua hausimami kabisa, ni binti mzuri lakini nilijaribu kufanya nikashindwa. Tulisumbuana sana lakini kwa aibu ya kuona kuwa nimeshindwa kufanya mapenzi nilimuacha akaondoka zake lakini sikua na amani kabisa. Nilitafuta mwanamke mwingine siku hiyohiyo nikajaribu kufanya nikafanikiwa, lakini katika kufanya mapenzi niligundua kitu kimoja, nilikua siwezi kufanya mapenzi kwa njia ya kawaida.

Kila nikifanya mapenzi njia ya kwaida uume wangu ulikua unalala, msisimko kulikua hakuna kabisa lakini kama nikimshika mwanamke makalio tu basi najisikia vizuri na kila kitu kinarudi kama kawaida. Mwanzo niliona kama kawaida kwakua kila mwanamke niliyekutana naye alikua ni wale wa kununua ambao walikua tayari kufanya chochote. Lakini nilipojaribu kuingia kwenye mahusiano na kutaka kufanya mpenzi kwa njia ya kwaida nilishindwa kabisa.

“Una matatizo gani?” Dada mmoja aliniuliza, alikua ni mfanyakazi Katika Benki moja hivi ambaye tulikua kwenye mahusiano kwa miezi kama mitatu hivi bila kukutana kimwili. Hata sijui, sijui leo ikoje….” Nilimuambia huku nikijaribu kumshika makalio ambapo ile kupitisha mkono wangu tu nilihisi kusisimkwa.
“Paaaaa!” Nilishangaa kaninasa kofi la usoni, kabla sijakaa sawa alinisukuma pembeni kwanguvu sana nikadondokea chini.
“Unataka kufanya nini, ndiyo nini kunishika hivyo makalio yangu!” Yule dada aliongea kwa hasira huku akinyanyuka.

Alikua kama kanitibua, nilihisi kama kanidhalilisha hivyo nilinyanyuka na kutaka kumfuata kumpiga, nilimmrukia pale kitandani huku nikimtukana.
“Malaya mkubwa wewe yaani unanisikuma mimi hivi unanijua!” Nilimuambia, lakini ni kama aliniona, alinikwepa sijui hata alinikwepaje, alisogea pembeni na kunyanyuka, mimi nilikua nimedondokea kitandani, hakunipa hata muda wa kunyanyuka, nikiwa pale chini alichukua kistuli kidogo cha kukalia na kunitwanga nacho mgongoni. Alinipiga kwa nguvu kiasi kwamba nilishindwa kunyanyuka.

“Mshenzi mkubwa wewe, yaani uhanithi wako ushindwe mwenyewe kufanya mapenzi halafu unataka kunipiga, hunijui wewe, sijwahi kupigwa na mwanaume yoyote na hakuna Mbwa hata mmoja atawahi nigusa!” Aliniambia huku akichukua nguo zake na kuanza kuvaa, wakati nikiwa bado naugulia maumivu nilianza kumtukana kuwa ni mbaya, malaya hana akili ndiyo maana nimeshindwa kufanya naye.

“Mbona nikiwa na wanawake wengine naweza, wewe unanuka huna akili ndiyo maana!” Nilimuambia, hata hakujali, aliendelea kuvaa zake taratibu huku akinigeuzia jicho kuniangalia namna nilivyokua naugulia mgongo. Nilijitahidi kidogo kujinyanyua ili kiumfuata, sikutaka kukubali kushindwa, nilitaka kumlipizia kisasi kwa kunipiga lakini niafadhali ningeacha.

Wakati nanyanyuka alikua ananiona, ile namsogelea ili kumvamia aliniwahi na teke kali katikati ya miguu. Aisee, hakuna maumivu ambayo nilishawahi kuyapata katika maisha yangu kama hayo, yaani nilihisi kama najifungua maana nilipiga kelele nikainama chini. Alivaa taratibu na kuondoka bila mimi kujua. Nilikaa pale chini bila kunyanyuka kwa masaa mawili mgongo unauma na hapa katikati kwenye zana zangu napo kunawaka moto.

Yalikua ni maumivu makali ambayo yalinifanya nisitamani kuonana na yule mwanmamke tena. Siku hiyo sikutoka kabisa, hata kula sikula mpaka asubuhi, yeye ndiyo alikua wakwanza kuniamsha, alinipigia simu kuniulizie naendeleaje.
“Wewe ni mshenzi nisikukamate!” Nilimuambia baada ya kupokea simu yake. Nilimtukana sana lakini yeye muda wote alikua amekaa kimya, mwisho aliniambia maneno ambayo yalinichoma kuliko hata maumivu ya lile teke.
“Utafikiri mwanaume anaongea, vitisho vyote hivi lakini nikivua chu*** unanywea!” Alikata simu na sikumtafuta tena, nilimblock na hata nikikuata naye njiani nilikua naona aibu, nilikua sitaki kuongea naye.

Maisha yaliendelea, tabia yangu ya umalaya sikuiacha kwani ilikua rahisi sana kwangu kupata wanawake katimka mitandao. Kwa muda sasa nilikua siwezi kutongoza kawaida, nikawa ni mtu wa mitandao masaa 24, niliacha kununua malaya na muda mwingi nikawa nautumia kwenye ngono ya mitandao. Kwakua mara kwa mara nikikutana na mwanamke nikijaribu kufanya naye mapenzi kawaida nashindwa hivyo wengine kuishia kugombana kwani hawataki kufanya mapenzi kinyume na maumbile niliacha kabisa kukutana na mwanamke.

Kila nikichart na mwanamke kwenye mitendao nataka tufanye phone sex, hiyo nilikua nafanya vizuri najichu ampaka nafika kileleni,. Niliizoe hiyo hali mpaka kila mwanamke nikipanga naye kukutana nilikua natafuta sababu. Walikua wananiamini kwasababu, kwanza nilikua nahonga sana, yaani mwanamke akiniomba pesa namtumia ili tu awe huru kunitumia picha zake za uchi. Pili nilikua naongea nao mpaka usiku, yaani hata video call ya saa nane usiku mimi nafanya hivyo mwanamke nikimuambia kuwa nampenda yeye tu na sina mtu mwingine sijaoa ananiamini hapohapo.

Kelele za kuoa zilizidi lakini hata sikujali, akili yangu ilikua ni kwa wanawake wa mitandao. Niliona kama ndiyo maisha yangu nilikaa kama mwaka hivi bila kukutana na mwanamke wa kawaida na niliona sawa. Nilikua najichua sana yaani nikiamka ausbuhi, nikiwa kazini mchana naweza kuingia chooni na simu yangu nikaanza kujichua na nikitoka kazini usiku nabadilisha tu wanawake wa kuwapigia simu kwwenye whatsapp wananiyonyesha maungo yao mimi najiridhisha.

Kila mwanamke niliyekua nikichart naye ilikua ni lazima kumuomnba picha za uchi, simu yangu ilikua imejaa mapicha ya wanawake zaidi ya mia tano ambao hata siwafahamu. Kuchart kwenye mitandao ilikua kama ndiyo kazi yangu, sikutamani hata wanawake wa kununua. Siku moja nikiwa kazini alikuja mwanamke mmoja, Salome (sio jina lake halisi) sikua nikimkumbuka, alinifuatilia mpaka kuja ofisini kwangu, mwanzo nilijua kama ni mteja lakini haikua hivyo.

Alikua ni mmmoja wa wanawkae niliokua nachart nao kwenye mitandao na mara nyingi alikua anaomba kuonana na mimi huku namzungusha. Kumbe alifuatilia mpaka kunipata, kusema kweli nilikua hata simkumbuki, nilikua na wanawake wengi na mara nyingi nawajibu kile wanachotaka kusikia na si kuwaangalia usoni.
“Imanaaana umenisahau wakati nishakutambulisha mpaka nyumbani kwetu, yaani mpaka Mama yangu anakujua, nilishakupa simu uongee na Mama yangu kweli hunikumbuki?”

Aliongea hukua kianza kulia, nikajua huu ushakua msala kwani suala la kutambulishwa kwa wanawake, kuongea na Mama wakwe ni wengi nilishaongea nao, wanawake wengi ukishatuma pesa mara mbili basi wanaona kama unawapenda, kwakua nachart nao mpaka usiku basi wanaona kama nawapenda hivyo suala la kuongea na ndugu ambao hata siwajui lilikua la kawaida sana kwangu.

Ili kuepusha kelele nilijifanya kama nimemkumbuka na kujifanya kama nilikosea.
“Aisee unaonekana mzuri sana uso kwa uso kuliko kwenye picha, yaani nahisi hata marafiki zako washawahi kukuambia, sikujua kama ni wewe….” Nililazimika kuzuga, wakati akiwa bado analia nilimfuata na kumkumbatia, nilianza kumsifia namna alivyokua ananukia, na kumuambia nashukuru kanitafuta na mambo kibao mpaka akasahau kama nilikua simkumbuki.

“Nimekuja kukaa kwako kama ulivyoniahidi…” Aliniambia.
“Ahadi gani tena jamani?” Niliwaza nikiwa sikumbuki kitu chochote.
“Nyumbani wanataka niolewe na mwanaume ambaye simpendi, nimewaambia kuhusu wewe hawataki wanasema ni kwanini huji, aisee nakupenda Sana G, nimekuja moja kwa moja maana nikikaa nyumbani ndoto zetu hazitatimia. Nimekuja si uliniambia niache kazi, niliongea na Afisa Utumishi akakubali waniandikie kama nimepunguzwa kazi ili niweze kupata NSSF yangu.”

Hapo ndipo nilichoka kabisa, akili ilikua haisomi, kusema kweli nilikua sijui kama nilishamuahidi hivyo, nachart na watu wengi na ni mara nyingi sana najibu meseji za wanawake bila kuzisoma vizuri lakini nyingi zilikua ni za mapenzi kama umekula, nimekumiss na si mambo ya kaucha kazi, kusema kweli nilichanganyikiwa kwani hata mwanamke mwenyewe nilikua simjui lakini alikua kaacha kazi kwenye kampuni moja kubwa sana kwajaili ya kunifuata mimi mume wake, mtu ambaye hata nilikua sijawahi kumuona, nilichoka kabisa.

MAMBO YANAKUA MAMBO; Unadhani George atafanya nini kuhusu Salome, unadhani wataona? Vipi kuhusu tendo la ndoa je ataweza kufanya naye? Salome ni nani na kwanini kachanganyikiwa sana kuhusu ndoa namna hii?

ITAENDELEA…. 

Post a Comment

Previous Post Next Post