SIMULIZI; AKIKUUA TUTAKUJA KUCHUKUA MAITI YAKO! 01----02

Natamani kumtaja jina lake lakini ni mtu ambaye anafahamika sana hivyo kaka naomba tu watu wasome kisa changu. Nimeamua kuandika kisa changu baada ya kusoma kisa cha David, watu wengi walikua wakimshangaa sana yule dada kwanini alikua anavumilia mateso yote yale. Niliposoma niliwashangaa sana watu kwani mateso aliyokua akipitia yule dada ilikua ni kama nusu ya mateso ambayo mimi mpaka sasa napitia. Niliposoma Comment za watu ndipo nilikumbuka maneno ya Kaka yangu ambaye aliniambia “Si unajifanya unampenda mume wako basi endelea kukaa naye akikuua tutakuja kuchukua maiti yako!”

Nilikutana na mume wangu miaka 10 iliyopita, wakati huo ndiyo nilikua nimemaliza chuo na tayari nilikua na ajira, yeye ni mfanyakazi wa shirika flani hivi na ana cheo kikubwa tu. Tulipendana na alikua ni mtu mzuri sana kwangu, mahusiano yetu yalidumu kwa miaka miwili ndipo alikuja kujitambulisha na kuleta posa. Hapo ndipo kila kitu kilibadilika, nakumbuka zilikua zimebaki wiki mbili tu kabla ya harusi, alinipigia simu kuwa anataka kuniona, tulipanga kukutana sehemu ya wazi tu kwani nisingeweza kwenda kwake kutokana na wageni wengi ambao walikuja kwaajili ya harusi.

Ilikua ni siku ya jumamosi hivyo nilikua tu nyumbani na wageni wageni. Tulipanga kuonana saa nane za mchana, lakini kabla ya kuondoka nyumbani ambapo hakukua mbali sana na sehemu tuliyokua tumepanga kuonana, Bibi yangu mdogo alikuja nyumbani, alikua ametokea kijijini akiongozana na mjomba wangu. yeye ndiyo nilikua nimechukua jina lake, na kwakua alikuja kwaajili ya harusi yangu basi ile salimia salimia ilinifanya kuchelewa kama dakika kumi na tano hivi. Niliaga na kwenda kumuona mchumba wangu, nilikuta ameshafika kaagiza na kinywaji.

Lakini hali yake ilikua ni tofauti sana, alionekana kuwa na hasira sana, nilihisi labda huko alikotoka ndiyo walikua wamemuudhi, nilifika na kuvuta kiti, nikamsalimia lakini hakuitikia, alianza kuangalia saa yake huku akiniangalia kama mtu aliyetaka kusema “Ndiyo saa nane hii?” niliwaza atasema na kweli alisema.
“Ndiyo saa nane hii? Hivi wewe ndiyo mtu wa kuniweka dakika kumi na tano nzima?” Aliniuliza kwa hasira.
“Samahani, Bibi alikuja nika….” Nilijaribu kujitetea lakini kabla sijamalizia alivuta chupa iliyokua mezani na kuipiga chini, ilipasuka na vipande kunirukia.

“Pumbavu, kwahiyo bibi yako ana umuhimu zaidi kuliko mimi? Hivi ulijua kuwa nimekuitia nini? Kama ningekua na tatizo kubwa, mimi ni mchumba wako, keshokutwa nataka kukuoa, je kama ningekua nimeahirisha ungekaa na huyo Bibi yako? Kama unamuona Bibi yako ni wamaana sana kwanini usingeenda akakuoa yeye!” Alifoka sana mpaka watu wakaanza kusogea na kuulizia nini kilikua kimetokea, niliishia kuwaambia hakuna shida kwani hata mimi nilikua sijui ni kitu gani kilikua kinaendelea kwenye akili ya mchumba wangu.

Alikua ni mtu tofauti kabisa, katika kipindi chote cha mahusiano nilimuona kama mtu mstaarabu, anayejali na mara zote alikua ni mtu wa kunisikiliza. Mara nyingi kila tulipokua tunakosana hata kama kosa lilikua ni langu basi yeye aliishia kuniomba msmaaha.
“Kuna nini kwani mbona mambo haya ni ya kuongea na kuyamaliza?” Nilimuuliza huku nikijaribu kumsogelea na kumshika bega. Hapo ndiyo nilikua nimefanya kosa la karine, nilimtibua haswa kwani aiukamata mkono wangu na kuuviringisha kama vile aanauvunja, maumivu niliyoyapata niliikuta najikojolea mbele za watu.

Nikiwa nimeinama chini kichwa nimekijunja bado kashikilia mkono wangu anaubinya, alichukua chupa nyingine ya bia na kunipiga nayo kichwani, alikua akinipiga huku akinitukana na kuniita Malaya, sina akili najifanya mzuri lakini anaweza kuniacha wakati wowote. Kwa bahati nzuri watu waliingilia, kaka mmoja ambaye baadaye nilikuja kujua kuwa alikua ni mwanajeshi alimshika na kuanza kumtandika makofi, alimpiga sana akimuambia kama ana nguvu apigane na wanaume wenzake si kupiga wanawake. Baada ya hapo alimchukua na kumpeleka polisi kisha akaondoka na kumuacha hapo.

Mimi sikujua kama kapelekwa polisi kwani baada ya kuachiwa niliondoka huku nikilia, nilifika nyumbani mkono unauma huku kichwani nimepasuka damu zinanitoka, watu waliokuepo pale walinishangaa na waliponiuliza niliwadanganya kuwa nimepata ajali ya Bodaboda. Walitaka kunipeleka hospitali lakini nilikataa, nilimuomba Mama aje ili niongee naye. Nilimuambia kila kitu kilichotokea mpaka mchumba wangu kupigwa na yule Kaka ambaye baadaye tulikuja kujua kuwa ni mwanajeshi.

“Kwahiyo mchumba wako sasa yuko wapi?” Mama aliniuliza.
“Mimi sijui aliponiachia nilimuacha akigombana na yule Kak…” Nilimuambia lakini kabla ya kumalizia Mama alinikatisha.
“Unaakili kweli wewe? Yaani mwanaume anakuoa wiki mbili zijazo lakini unamuacha anapigwa bila kujua hata hali yake, hukusimama hata kumtetea! Hivi wakimuua ndiyo utakua umepata faida gani, tutakua wageni wa nani? kwa hiyo hata hujui kuwa yuko wapi?” Alinishutumu na kuniuliza tena, nilikua katika maumivu makali lakini Mama hakujali, mkono ulikua unauma na nilikua nahisi kama vile umevunjika.

“Mtu umechelewa mwenyewe ulitaka kaka wa watu afanye nini? Kwani huyo bibi yako usingemsalimia angekufa? Ndoa hujaianza uhsaanza kumletea Kaka wa watu visa!” Mama alifoka hukua kiongea maneno ya kunichoma, hakujali kuhusu maumivu yangu alichokua akiwaza ni kuhusu mchumba wangu na kunishutumu kwa kila kitu. nilikasirika na kutaka kutoka kumuacha akilalamika lakini alinishika.
“Hivi una akili kweli, unataka kutoka na hiyop hali yako utasema nini? Unataka Baba yako akuone hivyo, hivi unafikiri watu wakijua tabia zako italeta picha gani? Kalisha matako hapo mshenzi mkubwa wewe…”

Alinishika na kunisukuma chini, alitoka na kufunga mlango kwa nnje, nilikua katika maumivu makubwa lakini maneno ya Mama taratibu yaliniingia, nilianza kujihisi kama mimi ndiyo mkosaji, nilianza kujihisi kama vile kuchelewa kwangu ndiyo kulimlazimisha mchumba wangu kunipiga.
“Inawezekana kweli, haat sio mtu wa vurugu, lakini na mimi nimezidi, singenipiga vile ila nisingechelewa na kumuongelesha vile asigenipiga, inawezekana ni kosa langu….” Niliwaza huku nikitembeatembea chumbani, nilichukua simu yangu kumpigia lakini ilikua imezimwa, nilijua labda kanizimia hivyo nilizidi kujisikia vibaya.

Usiku ule ulikua ni mrefu sana kwangu, kila wakati nilikua nikiangalia saa yangu ili kukuche. Mchana mzima sikupata taarifa za mchumba wangu na hata usiku, baadhi ya ndugu zake niliowapigia simu walikua hawajui alipo, nilipata wasiwasi sana. Mama alizidi kunichanganya, kila baada ya dakika kadhaa alikuja chumbani kwangu kuniulizia kama nimewasiliana na mwenzangu, nilimuambia kuwa simu yake ilikua haipatikani, alondoka kwa hasira.

Kichwa sehemu niliyokua nimepigwa chupa bado ilikua inauma, mkono ulikua umevimba lakini sikuyajali maumivu, nilikua na mawazo sana kuwaza alipokua mpenzi wangu. mpaka asubuhi nilikua sijasikia chochote, kwenye saa nne hivi simu yangu iliita, ilikua ni namba ngeni, nilipokea na ilikua ni sauti ya kiume.
“Wewe ndiyo Hilda (sio jina lake halisi)?”
“Ndiyo, ndiyo mimi Kaka…” Nilijibu harakaharaka, sikujua imetoka wapi lakini nilihisi kabisa ilitoka kwa mchumba wangu.
“Kuna mtu wako yuko hapa, anasema wewe ni mchumba wake, anahitaji mtu wa kumuwekea dhamana…”

Iliongea ile sauti, alikua ni askari na mchumba wangu alikua kapelekwa Polisi, nilijiandaa harakaharaka kwenda kumuona, nilitoka bila kuaga mtu yeyote kwani sikutaka maswali mengi, bado mkono ulikua unauma lakini kusikia habari za mchumba wangu zilinipa nafuu kidogo. Nilienda kituoni kwaajili ya kumuwekea dhamana, baada ya kukamilisha kila kitu alitoka na kuambiwa arudi kesho yake, hakukua na faili lolote lililofunguliwa lakini ilionekana kama mtu aliyempeleka pale ni mkubwa na alitaka tu kumkomoa.

Tuliingia kwenye gari mimi nikiendesha, njia nzima hatukuongea, nilitamani kumuuliza kilichotokea lakini alionekana kuwa na hasira sana, alionekana kuwa na mawazo mengi, nilitaka kumpeleka kwake lakini alikataa, aliniambia nimpeleke sehemu nyingine kabisa, tulienda mpaka kwenye nyumba moja, akafika na kugonga kwenye chumba kimoja, alitoka mwanamke, mbele yangu alimkumbatia yule mwanamke na kuanzana kupigana denda huku nikiangalia. Alinigeukia na kunipungia mkono kunionyesha ishara kuwa naweza kwenda yeye ameshafika.

Lakini sikwenda, nilitamani kukanyaga mafuta lakini mguu haukusogea, nilikua nikitetemeaka kwa hasira na uoga, kuona vile alikuja kwenye gari na kufungua mlango.
“Unasubiri nini? Ondoka au unataka kushuhudia kila kitu?” Aliniuliza kwa sauti kama ya kunishtua hivi. Macho yangu hayakua kwake bali kwa yule mwanamke, nilimuangalia nikijaribu kuvuta picha kama nilimuona wapi, sura yake haikua ngeni sana kwangu lakini nilikua sikumbuki nilimuona wapi?

Kama una rafiki yako ambaye anapenda Hizi simulizi basi mtag asijekupitwa na hakikisha unafollow na kulike ukurasa wanguSIMULIZI; AKIKUUA TUTAKUJA KUCHUKUA MAITI YAKO!---SEHEMU YA PILI

Nilishindwa kuwasha gari nakubaki namuangalia yule dada nikiwaza nilikua nimemuona wapi? Mara akili ilinijia, kuna siku moja nilienda ofisini kwa mchumba wangu nikakutana naye, hakua mfanyakazi mwenzake bali naye alikuja pale kumuona na ilionekana kama walikua wanagombana flani hivi, nilijaribu kumuuliza mchumba wangu kuwa ni nani lakini aliniambia ni mambo ya kikazi walitofautiana hivyo sikutaka kudodosa zaidi. Hasira zilinipanda zaidi kwani nilikua na muamini sana mchumba wangu na hata siku moja sikuwahi kufikiria kama anaweza kuchepuka.

“Nimekukosea nini lakini mpapa unaamua kunifanyia yote haya?” Nilikuta namuuliza, aliniangalia kwa dharau kisha akanijibu.
“Inaama huoni ulichonifanyia? Jana mimi nakuita lakini ukawaona ndugu zako kama ndiyo wa maana zaidi, umechelewa nakupiga kidogo unanijibu hovyo? Wakati nadhalilishwa na yule mwanaume wako si ulikuepo, sasa kwanini hukunitetea. Wewe ni kama mke wangu, keshokutwa nakuoa sasa kwanini hukusimama ukasema kuwa huyu ni mume wangu ukaachwa mpaka nikakaa ndani?” Aliniuliza kwa hasira, nilishindwa kumuelewa kwani kama ni tukio la kuchelewa lilikua ni la jana yake lakini yeye alishaanza kuchepuka zamani.

“Na huyo mwanamke, inaana ndiyo umempata hiyo jana wakati umelala polisi?” Nilimuuliza, alinyamaza kidogo kisha akanijibu.
“Wewe kipindi kile nakuambia unizalie si ulijifanya kuwa hutaki kuzaa, sasa wenzako wenye vizazi wamenizalia…” Nilishindwa kuendelea kumsikiliza, hasira zilinipanda na kuwasha gari kuondoka. Akili ilishanichanganya na niliona kuwa ile ndoa siwezi kuiweza.
“Siwezi kuvumilia kupigwa na mwanaume, hapana! Anipige halafu aende kuzaa na mwanamke mwingine!?” Nilijiongelesha, njia nzima niliendesha gari huku nikiwa nalia, niliaka tu kufika nyumbani na kumuambia kila mtu kuwa harusi imeahirishwa.

Nilifika nyumbani na kupaki gari, lakini kabla sijashuka Mama alikuja, ni kama alikua ananisubiria, kama alikua anajua kuwa naenda. Aliingia kwenye gari harakaharaka na kuniambia niwashe tuondoke. Niliktaa na kutaka kumuelezea kwanza kilichokua kimetokea lakini hakunipa nafasi.
“ondoka! Ondoka! Unataka kuniaibisha, hivi watoto wa siku hizi mmekuaje? Baba wa watu anapiga simu hapa analia, kalala polisi lakini wewe hata huoni? Hata kuomba msamaha umeshindwa eti uansema kupigwa? Kupigwa kitu gani? Mshenzi wewe unataka kila mtu aninyooshee kidole, ndoa zanyewe za shida umepata mwanaume anakuheshimu eti unalalamika kupigwa…!”

Mama aliongea kwa hasira, alinilazimishia kuondoa gari, alitaka niondoke pale. Njiani ndipo aliniambia kuwa mchumba wangu alikua amempigia simu anamuambia kuwa mimi nina hasira, tulitofautiana kitu kidogo lakini mimi nimechukulia hasira hiovyo nataka kuvunja uchumba. Alivyomshenzi alikua akiongea kwa kulia na kumuomba Mama kumuombea msamaha kwani inawezekana alikosea. Alibadilisha kisa kabisa, alimuambia Mama kuwa jana yake kuna sehemu tulikua tumekaa.

Kuna mwanaume mmoja akaja kunisalimia mimi kama vile tunajuana na yeye alihisi labda ni wapenzi, alipouliza basi yule mwanaume akapaniki na kuanza kumpiga, yeye akapigana na katika purukushani basi mimi nilipigwa chupa ya kichwa pamoja na kuniumiza mkono bahati mbaya kwani eti mimi nilikua namtetea huyo mwanaume. Baadaye polisi walikuja na kumchukua yeye kwakua huyo mwanaume ni askari mwenzao na mimi nikaondoka na huyo mwanaume. Mama alikua akiongea kwa hasira mpaka machozi yanamtoka.

Alishamuamini mchumba wangu, alishaamini kuwa aliyokua akiongea ni kweli kwakua kila mtu alikua akimuona mpole. Mchumba wangu alikua ni wale watu wakimya, haongei sana, mtu akiwa na tatizo humsaidia na huwezi kumkuta hata akibishana na mtu.
“Unakuja unalalamika umepigwa bila sbabau kumbe umefumaniwa? Kama una mwanaume wako na unafanya upuuzi wako kwanini uufanye mbele ya mchumba wako? Umeshindwa kumuambia huyo mwanaume kuwa wewe mchumba wa mtu akaheshimua hata uolewe! Haya Baba wa watu kafungwa umeenda huko umeleta vurugu unataka kuvunja uchumba unataka hao watu mimi niwaambie nini?”

Nilishindwa hata kitu cha kuongea, Mama alishaamini kila kitu, hata nilipomuambia kuhusiana na huyo mwanamke mwingine ambaye ana mtoto hakuamini, aliniambia ni maneno ambayo natunga kwakua nimemuona mwanaume wangu huko baaa hivyo nataka kumuacha mchumba wangu.
“Hata kama angekua na mwanamke mwingine nani wa kumzuia, huyo ni mwanaume, lazima awe na wanawake wengi, hivi unaona mimi na Baba yako tupo mpaka sas aunafikiri niko peke yangu. Nimevumilia mengi, ndiyo ndoa zilivyo, sasa unataka kumuacha mtu kwaajili ya mtoto, mbona una roho mbaya namna hiyo?”

Kabla hata sijamjibu Mama simu yangu iliita, alikua ni mchumba wangu, nikijua kuwa labda ataropoka kitu na kunitukana ili mama kumsikia, makusudi niliweka karibu na sikio la mama ilia sikilize.
“Mimi bado nakupenda, pamoja na yote uliyonifanyia lakini siwezi kuahirisha harusi kwasababu yoyote ile, naomba unisikilize, mimi ni mume wako hivyo nimekusamehe na nakupenda….” Hakuongelea kitu chochote kibaya alichokua kakifanya, aliongea maneno mengi ya kuonyesha kuwa mimi ndiyo mwenye tatizo simtaki hivyo anataka nafasi nyingine kwani hawezi kuniacha.

Nilijuta hata kumsikilizisha Mama yangu kwani ndiyo kwanza nilikua nimeupalia mkaa, alinitukana sana na kunionya, aliniambia kuwa kama nataka kumuacha mchumba wangu basi nijue kuwa yeye si Mama yangu. Alishuka kwenye gari na kuniambia kuwa uamuzi ni wangu, yeye kashaongea kamaliza hivyo hawezi kuongeza kitu kingine chochote kile. Mama alikua kapaniki sana, alitembea kwa mguu kama mtu aliyechanganyikiwa, ilinibidi kumfuata huku nikimuomba msamaha na kumuambia siwezi kumuaibisha.

Nilimuambia hivyo huku nikijipa moyo kwakuwaza kuwa labda kile kilikua ni kitu cha siku moja na mchumba wangu atajirekebisha. Nilijiongelesha mwenyewe maneno mengi sana kichwan, sikupata majibu ya maswali yangu yote lakini nilijipa moyo kuwa angalau labda akinioa hawezi kunipiga. Mama alipanda kwenye gari tukaondopka, njia nzima alikua akinihubiria kuhusu usiri, kufciha mambo yangu na nisiropoke ropoke kilichotokea hata kwa mashoga zangu, alinisihi sana na kuniabia kama nina tatizo basi nimuambie yeye na si kutangaza.

Nilimuahidi kumuambia, tukarudi nyumbani kama vile kulikua hakuna kitu klichotokea. Mchumba wangu alikuja nyumbani kuniona siku hiyo, alikua kawaida sana hakuonekana kujali, alinisalimia na kunichekea. Watu walipoondoka alinihakikishia kuwa hana mtoto bali alishawahi kuwa na mahusiano na yule dada lakini wakaachana na siku ile alinipeleka pale ili kuniumiza kama yeye alivyoumia eti kwa mimi kuacha kumtetea mbele za watu na kusema ni mpenzi wake, nilimsikiliza na kumkubalia ki shngo upande kwani nilijua kabisa ilikua ni uongo.

****

Mchumba wangu alibadilikanna kurudi kamja kawaida, kipindi chote cha sherehe alikua akiniomba msamaha na madai yake nikuwa nimekua nikimuudhi sana na kumfanyia dharau mara kwa mara ndiyo maana aliamua kunifanyia vile.
“Skupanga kukupiga, wewe mwenyewe unanifahamu nilivyo mpole lakini unajua kilichotokea, nilipandwa na hasira na wewe kama mwanamke ulitakiwa kujishusha.” Nilimsikiliza na kukubaliana na kila kitu alichokua anakisema, sikutaka kubishana naye kwani nilijua fika kama nikibishana naye basi anaweza kunipiga.

Kuhusu yule mwanamke aliapa kabisa kuwa hana mtoto naye na wala hana mahusiano naye. Bila mimi kumlazimisha alinipeleka mpaka kwa yule mwanamke na kumuuliza kama si wameshaachana, mwanamke alikubali na kusema kabisa kuwa hawana mtoto kwani yeye bado hajazaa. Niliridhika kidogo na kujipa moyo labda nikweli ila bado nilikua na wasiwasi kuhusiana na mabadiliko yake ya tabia. Hatusi iliendelea vizuri lakini niliumia sana kwani yule mwanamke alikuja na alikua akicheza makusudi kuniumiza.

Miezi mitano ya ndoa yetu ilikua ni mizuri sana, alikua ni mwanaume anayejali, mwanaume ambaye anapenda, mwanaume yule yule ambaye nilikutana naye kabla ya ndoa, yule ambaye alinitongoza na kunijali. Wakati huo nilikua nafanya kazi katika kampuni moja hivyo nilikua na kipato cha kutosha, tulikua tukishirikiana katika mambo mengi na uzuri nikuwa alikua najali, pesa yangu ilikua nadra sana kuitumia kwani yeye alikua akijitoa kwa kila kitu.

Baada ya miezi mitano ya ndoa nilipata ujauzito, nilipomuambia alifurahi sana, lakini hapo ndipo mambo yalianza kubadilika, alianza kuniambia nijiandae na kuacha kazi. Nilimuuliza ni kwa sababu gani akasema hataki mtoto wake kulelewa na mfanyakazi wa ndani hivyo mimba ikifikisha miezi sita nitaacha kazi kwani yeye ana kila kitu. Sikutaka kubishana naye sana, nilinyamaza lakini rohoni nilikua naumia, pamoja na yeye kuwa na kipato kikubwa mara tatu kuliko mimi lakini bado nilihitaji kufanya kazi.

Alikua ananihudumia kwa kila kitu sawa lakini kuna vitu vingi ambavyo nilikua nanunua mwenyewe na sikuhitaji kumuambia kuwa nataka kitu flani, kuna ndugu na marafiki ambao walikua wananiomba msaada na sikua na sababu ya kumuambia yeye. Maneno maneno yalianza, alianza kuchelewa kurudi nyumbani na lilipokuja suala la kufanya mapenzi alikua mkali.
“Wewe Malaya sana, yaani una mimba lakini bado unataka kutiw* tiw* ridhika unataka kuzaa mtoto wa nama gani?” Mara nyingi alinitukana tena bila sababu yoyote, niliishia kunyamaza na kujietea kuwa nilikua nafanya kwaajili yake.

Tabia yake ya kuchelewa kurudi nyumbani ilizidi, kuna wakati alikua akirudia subuhi na nikiongea naishia kupigwa, mwanzo ilikua ni makofi kawaida ila baada ya muda alianza kunipiga mateke bila kujali kama nimebeba mimba yake. Akishamaliza kunipiga basi akiniona nimekua mpweke hurudi na kuniomba msamaha.
“Unajua kuwa wewe ndiyo unanikasirisha, kwanini unapenda kuwa na kisirani namna hiyo? Mimi ni mume wako, ni mwanaume ni lazima uniheshimu, huna haja ya kunipigia pigia kelele kila siku, unanipangia maisha nikae na wewe na mimba yako hapa tufanye nini?” Aliniambia.

Nilinyamaza na kuomba msamaha, kila wakati nilijifanya kama mimi ndiyo mwenye makosa, sikua na mtu wa kumuambia, hakutaka niwe na marafiki akidai ndiyo huharibu ndoa za watu na kwa namna nilivyokua namfahamu Mama yangu niliogopa hata kumuambia kwani nilijua lazima atakua upande wake. Ujauzito ulipofikisha miezi sita alianza suala la mimi kuacha kazi, aliniambia mimi natakiwa kuandika barua ya kuacha kazi laini nilikataa na kumuomba asubiri mpaka nitakapojifungua.
“Unanipangioa? Unanipangia hivi hujui kama mimi ndiyo mwanaume humu ndani?” Aliniuliza, nilinyamaza bvila kumjibu lakini sikuacha kazi.

Niliendelea na kazi yangu lakini siku moja alikuja mpaka ofisini kwetu, akaingia kwa bosi wangu na kumuambia kuwa tumekubaliana kuwa mimi niache kazi, alileta barua ya mimi kujiuzulu akiwa kafoji saini yangi akamkabidhi bosi. Kwa bahati nzuri bosi wangu alikua muelewa sana, aliniita mume wangu akiwepo na kuniuliza kama nikweli. Kwakuogopa nilikubaliana nayeye kwani nilijua kama nitakataa basi anaweza kunipiga tena nikirudi nyumbani kwa madai ya kumdhalilisha.

“Una uhakika Binti?” Aliniuliza bosi wangu, yeye alikua ni baba mtu mzima, kuna kitu alikiona kwa mume wangu na alihisi kuwa labda sijashirikishwa.
“Nikweli bosi, nimekubaliana an mume wangu na mimi ndiyo nilimuambia ailete hii barua.” Nilijibu kwa uoga, mume wangu alisimama na kumkabishi barua kisha akaniambia nikusnaye vitu vyangu ili tuondoke.
“Hapana kijana, si kwa haraka namna hiyo, ngoja kwanza niangalie barua na tujue imekaaje?” Bosi alimzuia, mume wangu alisimama pembeni yake mpaka akaisoma yote.
“Umemaliza, kuna chakuongeza?” Alimuuliza, bosi wangu amabye naye alikua kasimama alikaa chini na kumuambia mume wangu naye kukaa.

“Kijana, kila ofisi ina taratibu zake, huyu binti anafanya kazi nyteti sana hapa, hawezi kuondoka tu hivi hivi bila kutoa taarifa. Hilada kama ulisoma mkataba wako wa ajira basi kunja kipengele kinasema kama unahitaji kuondoka bais unatupa notisi ya mwezi mmoja, lengo ni ili kutupa nafasi sisi kutafuta mtu mwingine. Umefanya kazi nzuri sana na ningeomba utuelewe kuwa ukiondoka yutakwama, lakini ukitupa muda basi mwezi ujao unaondoka, naja hali yako ila naamini kuwa unaweza kuvumilia angalau kwa mwezi mmoja?”

Bosi aliongea kwa utaratibu sana, mume wangu alimsikiliza kwa makini, pamoja na ushari wake lakini mume angua limuelewa na kuniambia kuwa ananipa mwezi mmoja na hiyo barua iwe kama notisi.
“Hilda wewe uasemaje maana wewe ndiyo mhusika mkuu hapa yusikuamulie?” Aliniuliza, nilimuangalia mume wangu kama vile naomba ruhusa ya kumjibu, kweli alikubali akaondoka na kuniacha kazini. Baada ya mume wangu kuondoka bosi wangu aliniita, alianza kunidodosa kwanini naacha kazi, sikua na jibu.
“Anakulazimisha?” Aliniuliza, nilinyamaza lakini alielewa, aliniambia hawezi kuniruhusu kuacha kazi kijinga jinga namna hiyo.

“Wewe ni kama binti yangu, mwanaume yeyote akijaribu kucheza na binti yangu basi nitamuonyesha namna ya kuwa mwanaume, kama anakupiga niambie, kama anakufanyia chochote kibaya niambie. Sitafuti mtu mwingine, utaendelea kufanya kazi hapa mpaka utakapochoka mwenyewe!” Aliongea kwa hasira, nilijaribu kujitetea lakini alikataa kunisikiliza.
“Akili zenu wanawake naziofahamu, mnaendeshwa e4ndeshwa na hivi vijanaume ambavyo vimepata pesa wakati havijabalehe vizuri vinajiona miungu watu! Kazi hutaacha na mwanaume akikuletea shida nitadili naye mimi!”

Nilitoka ofisini kwa bozi nikiwa nimechanganyikiwa zaidi, nilijua mume wangu atakasirika zaidi kama akisikia bosi ananitetea namna ile. Siku zilikua zinakimbia na mwezi ulipoisha mume wangu alikumbushia, nilimuambia bado ofisini hawajapata mtu lakini hakunielewa, alivumilia kwa wiki mbili hivi kisha siku moja alikuja ofisini kunichukua, alimuambia bosi wangu kuwa mimi ni mke wake na hataki nifanye kazi hivyo ananichukua. Bosi alikataa na alipotaka kuleta vurugu aliwaambia walinzi kumkamata na kumtoa nnje, mume wangu alikua mpole.

“Nitaondoka mwenyewe lakini naomba nimuambie huyo mwanamke, kuchagua kati ya mimi na kazi yake. Nikitoka hapo getini tafadhali usinitafute tena, itakua ndiyo talaka yako, sikulazimishi ila kama umeamua kuchagua kazi basi.” Aliongea huku akiondoka, nilimuangalia bosi kwa uchungu, alikua akinisihi kuwa nisikubali kunyanyaswa namna ile ila nilishindwa, niliamua kuondoka na siku iliyofuata niliwaletea barua rasmi ya kuacha kazi. Kila mtu alishangaa kwani walikua wananipenda sana nanilikua mfanyakazi bora sana.

Mume wangu alifurahia mimi kuacha kazi, alibadilika kwa kama wiki mbili hivi. Siku moja mimba yangu ikiwa na miezi nane nilipigiwa simu, ilikua ni jioni, mimi nilikua chumbani na sikujua kuwa mume wangu kasharudi toka kazini kwani aliingia kimya kimya. Ilikua ni sibu ya bosi wangu, alikua ananiuliz akama nina mpango wa kurudi kazini.
“Leo tumelazimika kufanya usahili kwaajili ya nafasi yako, kuna vijana wengi wana uwezo ila bado sijakata tamaa na wewe nataka uniambie kama tuijaze hii nafasi ua la? Kama hutarudi tena niambie maana kesho bodi inataka majibu na sijui cha kuwaambia. Nimewasubirisha sana kuwa umjamzito na mimba inasumbua ila watu wahsajua, mambo aliyofanya mume wako hapa imekua ngumu sana mimi kukutetea…”

Aliniambia, kumbe mume wangua likua anasikiliza na aliingia wakati huohuo kabla hata sijatoa jibu, kwa uoga baada tu ya kumuona nilijikuta namjibu bosi wangu kwa hasira.
“Nimeshakuambia sitaki kurudi, weka mtu mwingine mimi niko kwenye ndoa yangu na nina furaha na mume wangu…” Nilikata sim,u harakaharaka na kunyanyuka kumpokea mume wangu, lakini hata sikumfikia, nilikutana na teke la tumbo ambalo lilinisukuma na kujikuta napiga kichwa kwenye mbao ya kitanda.

Mume wangu alinivamia na kuanza kunipiga huku akinitukana, kusema kweli nilisikia masauti kama makelele makelele kwani kishindo cha kugonga kichwa kwenye mbao kilinifanya kuwa kama mtu aliyechanganyikiwa. Niliona marweruwe lakini nilisikia tu miguu yake na mikono yake ikinipiga, alinipiga mpaka nikapoteza fahjamu. Nilikuja kuzinduka saa tisa usiku, mwili umevimba nipo kwenye maumivu makali, nilijaribu kujinyanyua lakini nilishindwa, kila kitu kilikua kizito, tumbo lilikua linauma sana, nilijikuta nashindwa kufanya chochote na kulala palepale na maumivu yangu mpaka asubuhi.

Muda wote huo mume angua likua amelala kitandani, asubuhi aliamka na kuniamsha.
“Mwanamke mke wa mtu unalala mpaka sasa hivi unafikiri mimi kazini nitaendaje?” Aliongea kwa utani kama vile hakuna kitu chochote kilichokua kimetokea. Nilijitahdi kunyanyuka nikashindwa, alinishika mkono na kuninyanyua.
“Mke wangu na wewe kwa kujidekeza, kaugomvi kidogo tu unataka kusema huwezi kunyanyuka, sasa nani ataninyooshea? Leo chai ni kuywa ofisini tu…”

Alijiongelesha huku akiendelea kuchekacheka, kama kawaida yake baada ya kunipiga aliniomba msmaaha na kunilaumu, alikua akiniambia kuwa mimi ndiyo nimekkasirisha kwa kuongea na bosi wangu.
“Lakini nimependa jibu lako, mtu anaona tuna furaha anatraka kutuingilia, kwanini asimpe hiyo kazi mke wake…” Alijiongelesha, mimi sikumjibu, alitoa nguo zake na kuanza kuzinyoosha.
“Leo nakusiadia majukumu yako ila ukiendelea kudakadeka basi wenzako wapo wengi tu wa kukusaidia…” Aliendelea kuongea, mimi sikujali nilimuacha ajiongeleshe na kujijibu mwenyewe. Sikutaka kuingilia chochote kile mwili ulikua kwenye maumivu makubwa.

Maisha yaliendelea lakini siku mbili baadaye mtoto alikua ahchezi, nilienda kliniki kuwaambia, waliniuliza tangu lini nakumbuka ilikua ni mchana wa siku mume wangu aliponikpiga. Nilifanyiwa vipimo na kuambiwa niende hospitali kubwa. Kule nilipimwa na kuambiwa kuwa mtoto amefia tumboni.

Unadhani ni kitu gani kitatoke, kashaacha kazi kwasababu ya mimba, mtoto kafia tumboni, je mwanaume atajifunza na kuacha, nisikuchoshe hakikisha unafuatilia ukurasa wangu 

Post a Comment

Previous Post Next Post