SIMULIZI; AKIKUUA TUTAKUJA KUCHUKUA MAITI YAKO! 03---04



Hali yangu ilibadilika ghafla, ingawa mwanzoni walitaka nijifungue kawaida lakini ilionekana hali yangu ni mbaya, ili kuokoa maisha yangu walilazimika kunifanyia oparesheni na mtoto kutolewa. Alikua ni mtoto kamili kashakamilika kila kitu. Daktari ambaye alikua ni saktari wangu tangu mwanzo alishangaa ni kitu gani kilichokua kimetokea wakati mtoto alikua katika hali nzuri siku mbili kabla nilipoenda kiliniki. Nilishindwa kuongea nikimhofia mume wangu, mwanzo mume wangu aliniomba msamaha kwa kilichokua kimetokea akiniahidi kuwa hatanipiga tena.

Sikumuambia mtu yeyote kuhusu kupigwa na mume wangu, nilikaa kimya nikigulia kidonda changu na mume wangu kweli alibadilika kwa muda. Kutokana na kufanyiwa oparesheni niliambiwa kukaa angalau miezi mitatu kabla ya kufanya tena mapenzi. Baad aya kama mwezi mmoja tu hivi mume wangu alibadilika, alianza kuchelewa kurudi nyumbani na kuwa mtu wa hasira sana, kila nilipokua nikimuuliza alikua mkali, hakunipiga lakini alikua akiongea maneno ya kejeli na kunitukana nikalazimika kunyamaza.

Siku moja alichelewa kurudi, alirudi nyumbani akiwa kalewa sana, akaingia moja kwa moja mpaka chumbani, nilikua nishamuandalia chakula lakini hakula. Alikaa chumbani kwa kama nusu saa hivi simu yake ikaanza kuita, alikua kalala fofofo, ilikua ni namba mpya haikuseviwa, nilimuamsha ili kuipokea lakini alikua kalewa sana hata hakunisikia. Baada ya kuona ile simu inasumbua sana niliamua kuipoke aili kumuambia mpigaji kuwa mwenyewe alikua kalala. Lakini ile napoke atu nilikutana na matusi kutoka kwenye sauti ya kike.

“Mshenzi mkubwa wewe, yaani unaniacha kwenye gari unaingia kwako! Nususaa mimi nakusubiri mbwa wewe! unataka nifie humu ndani! Unatomb** kwanza na mke wako ndiyo uje kwangu…” Ile sauti ilitukana sana, nilishtruka kwani mhusika alimaanisha alikua nnje, bila kumuamsha mume wangu nilitoka nnje, nilienda mpaka kwenye gari ya mume wangu na kukuta kuna dada, binti modgo tu ambaye alikua kavaa vinguo vya kimalaya Malaya alikua kasimama ameshikilia simu.

“Unafanya nini nyumbani kwangu?” Nilimuuliza, aliniangalia kwa dharau huku akikata simu.
“Kwako hapa? Wewe si kama mimi tu umeweka, umechangia tofali hap…” Alianza kuongea kwa dhara, nadhani zilikua ni hasira za mume wangu kunifanyia yote yale, nilijikuta namshika nyywele na kuanza kuzivuta, alipige kelele nyingi za maumivu huku akilia kuwa nimuachie. Nilivuta mpaka getrini, mlango mkubwa ulikua wazi kwani mume wangu alipoingia hakuufunga, ilionekana walishapanga kutoka tena na ndiyo maana yule dada alikua anmsubioria, nilimtoa nnje na kufunga geti langu.

Lakini ile narudi ndani mume wangu alikua kashatoka, alionekana ndiyo kwanza alikua kazinduka kutoka usingizini. Hakunisemesha chochote alitoka na kuingia kwentye gari, hakumuona yule Dada hivyo alikuja kwangu na kuniuliza nimefanya nini? Nilimuambia nilichofanya, bila kusema chochote alininyang’anya simu yake, alienda na kufungua geti akaingia kwenye gari na kutoka. Sikumuona tena mpaka siku iliyofuata, alirudi nyumbani saa tano asubuhi, alikua hajalewa yuko kawaida.

Ingawa nilikua na maswali mengi sana kichwani kwangu lakini sikumuuliza, nilijua kuwa haitasiadia kitu, alishaamua kuchepuka hivyo niliamua kumuacha na maisha yake.
“Mbona huniulizi chochote?” Aliniuliza baada ya kuingia ndani na kukaa kama nusu saa bila mimi kumuuliza kitu kilichotokea jana yake.
“Nikuulize kuhusu nini?” Nilimuuliza kwa mshangao, nilijua kabisa anataka kuleta gubu hivyo niliongea kwa sauri ya chini.
“Wewe utakua na wanaume wengine, haiwezekani mume wako anachepuka anakuja na mwanamke mpaka nyumbani lakini husemi chochote, hembu niambie, au unataka kuniua?”

Nilimuangalia kwa hasira nikitamani hata kumpiga na chupa ya chai ambayo ilikua mezani, mimi niliamua kunyamaza lakini kwake hilo nalo lilikua ni tatizo.
“Mume wangu unataka nini kwangu? hivi kweli unataka mimi niwe nakuchunga kama mtoto, wewe ni mtu mzima, una akili zako, unataka nihangaike na wewe?”
“Inamaana hunionei wivu, kama hunionei wivu basi utakua hunipendi, wanawake wengine wangegombana lakini wewe umekaa tu, nahisi hunipendi, siwezi kuishi na mwanamke kama wewe, kama huwezi hatakunionea wivu mimi naona kabisa bora tuachane!”

Aliongea kwa suti ya chini kidogo huku akinisogelea na kutaka kunishika, hapa aliongea kama kautani kidogo lakini kwa kumaanisha. Nilijisogeza pembeni, sikutaka aniguse kabsia. Kitendo cha kujisogeza kilimuudhi, alianza kulalamika na kusema kuwa simtaki kimapendi ndiyo maana anamaua kuchepuka.
“Mume wangu mimi nina mshono unatraka nianze kufanya mapenzi? Kweli ni haki hiyo?” Nilimuuliza, alikasirika zaidi na kuniambia kuwa kuna wanawake wengi wanakua na miishono tena mikubwa kuliko wangu lakini wanafanya mapenzi na waume zao.

“Mimi nimchoka kuchepuka, nakutaka mke wangu na nataka kufanya mapenzi na wewe, kama huwezi basi ondoka nyumbani kwangu, kwani kinachofanya mpanzi ni tumbo au?” Nilinyamaza kimya bila kumjibu, kitu ambacho kilimfanya kulalamika zaidi kuwa simpendio na nina kiburi. Alinichosha na kunipendisha hasira, bila hata kupanga nilijikuta nanyanyuka na kuondoka nikimuacha kakaa peke yake sebuleni, niliingi chumbani, sikua na kitu cha kufanya huko lakini niliingia ili tu kumkwepa mume wangu.

Hicho nacho kilimkasirisha mume wangu, alikuja kitandani na kunivamia, alinishikilia chini na kunilazimishia kufanya mapenzi, hakujali mshono, hakujali maumivu yangu na hakujali chochote kile. Nashukuru Mungu pamoja na kunifanyia kwa nguvu tena akifanya makusudi ili kuniumiza lakini sikuumia, hakunitonesha mshon, alifanya anavyotaka na kuanzia siku hiyo ilikua kama kazi, alikua akiniambia kuwa anataka mtoto na kwakua yule mwingine nimemuua makusudi basi hataki kusubiri.

Niliumizwa na vitendo vyake lakini niliumizwa zaidi na maneno yake, namna ambavyo alikua anaongea ni kana kwamba mimi ndiyo nilisababisha mimbayangu mtoto kufia tumboni.
“Tatizo lako unapenda kunikasirisha sana, ungekua na nidhamu sidhani kama mtoto angefia tumboni, wala nisingekupiga, sikudhamiria kukupiga!” Alikua akiniambia, kwa namna alivyoongea kuna wakati nilijihisi kabisa kuwa labda tatizo ni mimi, niliona kabisa kuwa mimi ndiyo nilimsababisha mume wangu ili kunipiga, kuna wakati nilipiga magoti na kumuomba Mungu msamaha kutokana na dhambi ya kuua.

***

Miezi mitatu baada ya mimba yaangu ya kwanza kuharibika nilikua na ujauzito mwingine, bado nilikua Mama wa nyumbani sina kazi, manyanyaso yalikua mengi lakini nashukuru Mungu niliweza kujifungua salama. Katika ujauzito huu mume wangu hakuninyanyasa, si kwasababu alikua anapenda, hapana nikwakua Mama yake alikua pale nyumbani. Mama yake alikua anaumwa hivyo alilazimika kuja kutibiwa, mume wangu ni wale watu wakupenda kujionyesha kuwa wanajali, wanapenda na kutaka kuonekana wema.

Kwa sababu hiyo Mama yake alikuja kipindi nina ujauzito wa miezi miwili, nilimhudumia mpaka nilipofikisha miezi sita alipona lakini alikataa kuondoka akinihudumia na mimi kwani alikua akiamini kuwa sababu ya mimi kumpoteza mtoto wangu wa kwanza ni kazi nyingi hivyo kwakua alikua nha hamu sana na mjukuu basi angekaa mpaka nijifungue. Kweli nilijifungua salama na mtoto alipofikisha miezi mitatu Mama mkwe aliondoka na kurudi kijijini kwao. Mume wangu ndiyo alimpeleka na ni kama alikua anasubiri Mama yake kuondoka ndipo aanze vituko vyake.

Ingawa alisema kuwa atakaa siku mbili lakini mume wangu alikaa siku sita, hakua kwao kwani Mama yake aliniambia kuwa ashaondoka. Alikua akinipigia simu kuniulizia kuhusu mtoto ila nilipomuuliza alipokuepo basi ilikua ni ugomvi kuwa nataka kumkalia kichwani yeye ni mwanaume na hapangiwi. Niliishia kunyamaza na aliporudi hata sikumuuliza. Maisha yaliendelea lakini mume wangu alianza kuwa mbahili, alikua hatoi pes aya matumizi, alimfukuza mfanyakazi wa ndani kwa madai kuwa mimi ni Mama wa nyumbani sina kazi ya kuhitaji mfanyakazi.

Alikua ni mtu wa kukaa mpaka siku tatu nne harudi nyumbani, haachi pesa ya chakula na nikiuliza tu ni matusi na vipigo. Nilitumia kila akiba niliyokua nayo mpaka ikaisha, mume wangu hakua anahudumia chochote, alinitelekeza na akirudi nyumbani alikua akihitaji chakula kama kawaida. Hali ilikua ngumu zaidi kwani mafao yangu ambayo nililipwa kazini aliyachukua kinguvu nikabaki sina kitu kabisa. Baada ya kuona hali inakua ngumu sana niliamua kutafuta kazi, nilizunguka sana kutafuta kazi kimya kimya bila mume wangu kujua lakini kazi nazo zilikua ngumu.

Nilizunguka sana bila mafanikio kwani kila sehemu nilipokua nikienda basi nilikua nikikataliwa kutokana na kuwa na mtoto mchanga. Baada ya kuzunguka sana kutafuta kazi za elimu yangu nilichoka na kuamua kutafuta kazi yoyote ile bora nipate hela ya kula kwani mume wangu alikua hajali, alikua anaweza kukaa hata wiki bila kurudi nyumbani, kujua nakula nini wala mwanae anakula nini. Nilipata kazi ya kufua, nilikua nikizunguka kwenye majumba ya watu, nawaomba kuwafulia na kufanya usafi wananilipa elfu kumi au siku nyingine tano na siku inaisha.

Siku moja nilikua nafua sehemu, wakati nafua kuna gari ilikuja na kusimama, ukiwa kwa ndani mlango mdogo wa geti ukiwa umefunguliwa basi unaona nnje, niliona lilikua na nembo ya gari la ofisi yangu ya zamani, sehemu niliyokua nikifanya kazi. Walishuka wakaka wawili, wote sikuwafahamu, waliingia katika vyumba vya jirani na yule mtu niliyekua nikimfulia, walikaa kama dakika kumi hivi ndipo aliingia mzee mmoja, huyu nilimkubuka kwani alikua ni dereva, tena dereva wangu kipindi nafanya kazi. Nilipomuona anaingia nilijigeuzia ukutani kwani sikutaka anione.

Alienda kwenye chumba cha wale wakaka na kuongea nao kitu kisha wakatoka, wakati anatoka alimuona mtoto wangu ambaye ndilikua nimemkalisha kwenye karai nimemuwekea na nguo kwani alikua bado hajaanza kukaa vizuri. Mtoto alipowaona alianza kulia tena sana, niliendelea kujibanza ili watoke nimchukue mtoto wangu lakini hawakutoka, walisimama na yule mzee alianza kumbembeleza mtoto, alimuangalia na alipombeba mtoto alinyamaza kimya kama kashikiliwa na Baba yake.

“Wewe ndiyo Baba nini? Mbona kakupenda ghafla?” Wenzake walimtania, alicheka huku akinifuata kunipa mtotyo.
“Dada mwanao atakua na njaa ndiyo maana analia…” Aliniambia sikua na namna zaidi ya kugeuka, nilikua nimchoka sana ukilinganisha na mwanzoni. Mwanzo hakunigundua kwani hakudhani kuwa anaweza kunikuta maeneo kama yale,. Alinikabidhi mwanangu lakini kabla ya kutoka alikumbuka kitu na kugeuka.
“Dada samahani…” Alikua ni mzee mtu mzima lakinia liniita Dada, hakuniita hata mwanangu kwa namna nilivyokua nimchoka.

“Kuna Binti mmoja umefananana naye, anaweza kuwa mdogo wako au ndugu yako, mmefanana sana, mtu angeweza….” Hakumalizia, alinyamaza kidopgo kisha akaniangalia tena na kuniambia.
“Hapana, niwewe Bosi? Si Hilda wewe?” Nilitamani kumuambia kuwa amenifananisha lakini nilishindwa.
“Haya ni maisha tu kwanini nijionee aibu?” Niliwaza na kuamua kumuambia ukweli kuwa ndiyo mimi. Alikua na maswali mengi lakini aliitwa ikionekana kuwa mabosi wake wana haraka, aliondoka huku akiniachia noti ya Shilingi elfu kumi. Nilimshukuru sana kwani alikua kanisaidia sana.

Niliiangalia ile elfu kumi machozi yakanitoka, miaka miwili nyuma yeye ndiyo alikua anakuja kwangu kunililia matatizo ya familia yake na mimi kumpa elfu kumi sasa hivi yeye ndiyo alikua ananipa. Nilimshukuru sana Mungu kwa siku hiyo. Nilimalizia kufua na kurudi nyumbani, lakini jioni simu yangu iliita, ilikua ni namba ya Bosi wangu wa zamani, nilikua naijua kichwani, nilipokea baada ya salamu aliniambia kuwa kesho yake niende ofisini kumuona. Sikujua alipata wapi namba yangu kwani ilikua ni mpya lakini kesho yake nilikua ofisini kwake.

Tuliongea mengi, nikamuambia baadhi tu ya mambo ambayo yalinitokea katika maisha yangu namna nilivyopoteza mtoto na sasa hivio hali ni ngumu kwani mume ni kama kanitelekeza.
“Ile nafasi yako kwa sas ahaipo ila kuna nafasi za chini chini, unaweza kuanza huko huku tukikutafutia nafasi ya hadhi yako.” Nilisita kuchukua ile kazi nikiwaza kuhusu mume wangu lakinia liniondoa wasiwasi akiniambia kuwa mwanzo aloifanya makosa kuniacha niondoke ila si sasa.

“Huyo mume wako kama ni mwanaume kweli atapambana na mimi, niachie hiyo kazi hataongea chochote.” Aliongea kwa kujiamini, nilikubali ile kazi na kuanza, sikumuambia mume wangu kwani hakuepo nyumbani. Lakini sijui ni nani alimuambia kuwa nafanya kazi ila siku tano baadaye alikuja nyumbani na kunifukuza akisema kuwa natembea na Bosi wangu, nilimpuuzia na kumuambia kuwa sina mahusiano na Bosi wangu lakini hakuamini, aliniambia kuwa hanitaki. Kwakua nilikua na kazi sikujali sana, niliondoka na kwenda kulala Gest na mwanangu kwani nilikua naenda naye kazini.

Nilikua bado sijapata binti wa kazi hivyo kwakua hata bado nilikua sijapata kazi maalumu basi niliruhusiwa kumpeleka. Siku iliyofuata nilipanga kutafuta chumba ili nianze maisha upya kwani nilishachoka manyanyaso ya mume wangu. Lakini usiku nilipokea simu kutoka kwa mke wa Bosi wangu akiniambia niachane na mume wake. Mimi nilishangaa kwani sikua na mahusiano na Bosi wangu lakini yeye aliniambia kuwa anahabari kuwa nimemkimbia mume wangu kwaajili ya mumewe hivyo nikae mbali naye.

Alikata simu kabla ya hata mimi kujielezea. Usiku huo sikulala nilibaki na mawazo sana nikiwa sijui hatima yangu. asubuhi kama kawaida nilienda kazini, kwenye saa nne hivi niliitwa ofisini kwa Bosi na nilipofika nilimkuta mkewe kakaa kakasirika.
“Kwanini una mkingia kifua kama si hawara yako, anafanya nini hapa? Ni eidha mimi au huyo mwanamke wako, huwezi kumng’ang’ania mke wa mtu anakuhusu nini?” Wakati naingia mke wa bosi alikua akilalamika na bosi akimsikiliza.

 Nadhani sina haja ya kukuambia kuwa sehemu ya Nne inapatikana katika ukurasa wangu tu bontyeza hapa 

SIMULIZI; AKIKUUA TUTAKUJA KUCHUKUA MAITI YAKO!---SEHEMU YA NNE

Mke wa bosi wangu alikua kafura, alikua kama mtu aliyechanganyikiwa akimshutumu bosi wangu kwa kutembea na mimi. Nilitaka kuongea kujielezea lakini Bosi wangu aliniambia kunyamaza.
“Sikukuita hapa ili ujielezee, hapana, mke wangu hahitaji maelezo yako ili kuniamini.” Aliongea na kutulia kidogo, mke wake aliniangalia kwa hasira. Bosi alinimuambia mke wake akae, alikataa lakini alimkazia macho mpaka akakaa.
“Naataka umuangalie huyo binti vizuri…” Aliongea, mke wake aliniangalia tena kwa dharau zaidi.
“Una miaka mingapi?” Aliniuliza, nilifikiri kidogo kisha nikamjibu.
“34, ndiyo nimefikisha juzi.”

“Mke wangu, Asha ana miaka mingapi?” Alimuuliza mke wake ambaye hakuonekana kama kumuelewa.
“Asha?”
“Ndiyo, Asha mtoto wetu.”
“Mhhh! Atakua na 27 au 28, mimi sikumbuki vizuri.” Mke wake alijibu huku bado akinikazia macho.
“Ana miaka 26 ila keshokutwa anaingia 27. Na suisi tumekaa kwenye ndoa yetu kwa miaka mingapui?” Alimuuliza na mke wake alimjibu miaka 35. Bosi alitabasamu kisha kuniambia kuwa niondpke, kabla sijaondoka mkewe alilalamika kuwa natakiwa kufukuzwa kazi ndipo Bosi alimuambia.

“Unanifahamu kwa zaidi ya miaka 40, tangu tunakutana kijijini mpaka nakuoa. Kama katika miaka yote hiyo basi unaweza kuamini maneno yam pita njia kuwa mimi naweza kufanya mapenzi na mwanamke sawa na binti yangu basi mke wangu hunijui vizuri na sidhani kama kuna maelezo yoyote ambayo naweza kukuambia yakawa na maana. Kama umekaa na mimi miaka 37 kwenye ndoa tunalala na kuamka pamoja lakini huwezi kuniamini unaamini simu moja ya mpumvavu mmoja basi nadhani sina haja ya kukuelezea sana, tukifika jioni nitachukua vitu vyangu nitaondoka kwani kama huniamini sidhani kama mimi ni mtu sahihi kwako.”

 Bosi aliongea kwa uchungu sana mpaka mke wake akaanza kuona aibu na kuanza kujitetea.
“Lakini wanaume wanabadilika mume wangu…” Aliongea kama vile anabembeleza.
“Wanabadilika ila naamini unanijua vizuri sana mke wangu, kuna mambo unajua naweza kuyafanya na mambo ambayo unajua siwezi kuyafanya. Labda nakuhukumu bure, lakini naomba utoke na huyu binti kaongee naye kisha urudi hapa halafu uniambie hivi kweli kama kuna mwanaume angekua anamfanyia binti yetu mambo kama haya usingemsaidia huyu binti?” Bosi aliongea huku akituonyeshea ishara ili tutoke.

Nilitoka na mke wa Bosi mpaka ofisini kwangu, aliniambia nifunge mlango, mwanzo nilihisi kuchanganyikiwa nikidhani labda kuna kitu kibaya anataka kunifanyia lakini alinitoa hofu.
“Usiogope, namfahamu mume wangu, nilipaniki kidogo lakini namfahamu mume wangu, naomba uniambie kuna nini.” Nilifunga mlango na kukaa kisha nikaanza kumuelezea mke wa bosi mataizo yangu, nilimuambia kila kitu bila kuficha, namna mume wangu alivyokua akinipiga na kuninyanyasa, namna ambabyo mimba yangu ya kwanza mtoto alifia tumboni, nilimuonyesha makovu ya viboko mgongoni, nilimuonyesha mistari ya viboko kwenye mapaja na mateso mengine mengi.

Wakati wote huo alikua akilia, tulitoka pale mpaka kwa mume wake, alimuomba mume wake msamaha na kumuambia kuwa nahitaji kuondoka kwa mume wangu, alimuambia wanaipe nyumba ili nikakae wakati nikijipanga lakini bosi alikataa.
“Huyu ni mtu mzima anapaswa kufanya maamuzi yake mwenyewe, kama anataka kuondoka basi hatupaswi kumpa nyumba, hapana atabweteka, anahitaji kuwa na kwake. Tutamlipia kodi ya miezi sita ksiha ataendelea mwenyewe na maisha yake kama wafanyakazi wengine.”

Alinipa muda wa kutafakari, kwakua nilishapanga kuondoka sikua hata na kitu cha kutafakari, baada muda nilimuambia nataka kuondoka, walinitafutia chumba na sebule wakaniambia nianze maisha sehemu amayo mimi nitakua na uwezo nayo kutokana na kipato changu. Niliondoka na kuhama bila kumuambia chochote mume wangu, alikua hayupo nyumbani kama kawaida yake. Baadaye alijaribu kunitafuta na kuniletea vurugu lakini Bosi alsihanipanga, nilienda Polisi na kwakua Bosi naye alikua akijulikana kama mume wangu walipambana na mume wangu akanywea na kuniacha niendelee na maisha yangu.

Maisha yalianza kuwa na amani nikiishi mimi na mwanangu, mume wangu alianza kuhangaika kwa ndugu na kutangaza kwa watu kuwa nimemkuimbia na kuiacha ndoa lakini sikujali, nilishaamua kuandelea na maisha yangu sikutaka kitu chochote kile kunisimamisha. Baada ya kuona kuwa sitetereki mume wangu alikata mawasiliano kabisa, alikua hahudumii mtoto chochote, hatoi matumizi wala hapigi simu kuulizia hali zake. Mimi pia sikujali na wala sikuulizia chochote, nilifanya kazi kwa bidii mpaka kupanda cheo na kuwa na cheo changu cha awali hivyo nikawa niko vizuri.

Baada ya kuona niko kimya naendelea na maisha yangu mume wangu alianza kunitafuta, alipitia kwa ndugu zangu, alianza kwa Mama yangu akimuomba kuongea na mimi. Alimuambia kuwa amejirudi na kuna mambo ambayo alikosea huko nyuma. Mama Alinitafuta, nilimuambia kilichotokea lakini hakujali.
“Mwanaume akikuomba msamaha unamsamehe, wewe ushakua mtu mzima, unafikikiri kuna mwanaume mwingine atakutaka kama ukiachika, vumilia mwanangu, mume wako ni msomi, ana kazi nzuri na anapesa sasa kwanini kuhangaika huko na vinyumba vyakupanga, kama mwanaume kakuomba msamaha basi msamehe.”

Mama aliniambia, kwangu ilikua ngumu sana kurudiana na mume wangu, Baba yangu hakua akijua kilichokua kikiendelea lakini aliniambia uamuzi ni wangu kwani mimi ndiyo nilikua naenda kuishi naye. Wadogo zangu na Kaka zangu sikuwaambia chochote, walijua tu tumegombana kawada. Mwanzo niligoma lakini baada ya mume wangu kutuma ndugu zake na kuapa kuwa hatarudia basi nilikubali kumsamehe. Aliniruhusu kuendelea na kazi na maisha yaliendelea. Mume wangu alibadilika kabisa, hakunipiga tena, alihudumia familia na kweli niliona kabisa kuwa ni mtu mpya.

Nilipata ujauzito wa pili na kujifungua salama, mtoto akiwa na miezi sita nilipata mimba nyingine, mume wangu alitaka nizae harakaharaka lakini mimi sikutaka, bado mwanangu wa pili alikua mdogo, nilitamani kuitoa mimba lakini baada ya kuongea na Mama aliniambia watoto ni baraka hivyo nizae tu. Baada ya kubeba ujauzito wa tatu mume wangu alianza kurudia hali yake ya zamani, alianza kuchelewa, alianza kuninyanyasa na maneno mengine ya kashfa kibao tu. Alitaka niache kazi lakini mimi sikua tayari kusha kazi, kisingizio chake kikubwa ilikua ni watoto wake, hakutaka wanae kulelewa na binti wa kazi.

Siku moja nilikua nimetoka kazini, nilikua nimchoka sana hivyo nilivyorudi nyumbani sikufanya chochote, moja kwa moja nilielekea mpaka chumbani kujilaza baada ya kumnyonyesha mtoto. Nikiwa nimepitiwa na usingizi niliamshwa na kelele za mtoto akilia. Mtoto wangu wa kwanza alikua kwa Bibi yake, hivyo nilikua na mtoto mchanga tu ambaye baada ya kumnyonyesha nilimlaza katika kitanda chake chumbani sebuleni kwani mchana tunakisogeza sebulani ili iwe rahisi dada wa kazi kumsikia.

Mtoto alikua analia sana kiasi cha kuniamsha mimi ambaye nilikua chumbani. Nilitoka na kumchukua, nilianza kumtafuta dada wa kazi ili kujua ni kwanini alikua anamsikia mtoto analia lakini hamhudumii. Nilizunguka sana ndani kote sikumuona, nilitoka mpaka nnje lakini sikumuona. Wakati nataka kurudi ndani niliona gari ya mume wangu ikiwa imepaki, nilishangaa kwani wakati naingia mume wangu alikua bado hajarudi, mlango wa nyuma ulikua umefunguliwa, nilijua mume wangu yupo hivyo nilienda kumuangalia na kumsalimia kwani nilihisi labda ndiyo anaingia nyumbani na huenda anavitu vya kubeba ndiyo maana kafungua mlango wa nyuma.

Nilitembea taratibu, ile nafika tu nasofeza mlango, nilimkuta mume wangu kainama, kashusha suruali mpaka chini kwenye magoti anafanya mapenzi na binti yangu wa kazi. Aliponiona hata hakushtuka, aliendelea kufanya binti wa kazi hakuniona kwani yeye alikua amelala chini. Nilitamani kupiga kelele lakini nilishindwa, nguvu ziliniishia nikadondoka chini nikiwa na mtoto mkononi. Sikupoteza fahamu hivyo nikiwa pale chini sina nguvu hata ya kunyanyuka nilimuona mume wangu akiendelea kufanya mapenzi na binti yangu wa kazi tena mbele yangu. ilikua ni jioni tu kigiza ndiyo kinakaribia kuzama hivyo kila nikifungua macho niliona kila kitu.

Alifanya mpaka akamaliza huku mtoto akiwa mikononi mwangu akilia, baada ya kumaliza alimchukua mtoto na kuingia naye ndani wakaniacha pale nikiwa chini. Baada ya kama nusu saa hivi nguvu zilinirudia, nilinyanyuka na kuingia ndani, nilimkuta binti wa kazi kajifunmgia chumbani analia, mume wangu kakaa sebuleni anmambembeelza mtoto. Kwanza nilimchukua mwanangu sikutaka ambemende, nilimpeleka chumbani na kumlaza kisha nikarudi mpaka kwenye chumba cha yule binti, nilianza kugonga mlango nikimuambia afungue, nilitukana na kutukana lakini hakufungua, mume wangua linifuata na kunipiga makofi.

“Wewe ndiyo umeyataka yote haya, mimi nilioa mke wa kunifulia na kunipigia, sasa kama huwezi makujumu yako kama mke kwanini wenzako wasikusaidie, kwanini unachagua kazi za kusaidiwa nazo na nyingine hutaki?” Aliniuliza kwa makofi, mume wangu alinipiga sana hakujali hata kama bado nimjamzito. Alinipiga sana na kuniambia kuwa hata nikimfukuza yule binti nikaleta mwingine naye atatemeba naye na kama nataka aache kutembea na mabinti wa kazi basi niache kazi na kumhudumia yeye kama mwanaume kwa kila kitu. Nililia sana lakini hakujali, aliniambia hawezi kuishi na mwanamke ambaye atembei naye.

Pamoja na yeye kuongea sana na kukataa nisimfukuze lakini asubuhi yake nilimfukuza yule binti nyumbani kwangu. Sikua na mpango wa kuacha kazi lakini nilikua na mtoto mdogo, nisingeweza kumpeleka kazini kwani mikiki mikiki ya kazini ilikua mingi. Nilimpeleka kwa wifi yangu wakati nikitafuta binti mwingine wakazi. Nilihangaika kutafuta binti wa kazi nilikosa ambaye angekua na vigezo vyangu, sikutaka kuacha kazi hivyo nilitaka kutafuta mwanamke mtu mzima ambaye mume wangu asingemtamani.

Baada ya kama miezi miwili ya kuhangaika nilipata, mume wangu alikasirika kwani alikua ni mama mtu mzima lakini sikujali, nilichotaka ni kulinda ndoa yangu na kuendelea kufanya kazi kwani nilijua kuwa kama nikiacha kazi manyanyaso ya kipindi kile yatarudi. Maisha yaliendelea, manyanyaso hayakupungua, mume wangua likua hampendi yule Mama hivyo hasira zake zote alinishushia mimi, alikua ni mtu wa kuchelewa kurudi, alikua ni mtu wa kunipga na kunitukana matusi ya nguoni kwa lengo la kunidhalilisha, vyote hivyo nilivumilia.

Siku moja mume wangu alikuja na kijana mmoja, alikua ni kijana mdogo tu labda wa miaka 22, aliniambia kuwa ni mdogo wa rafiki yaake, mimi nilimpokea na kumkaribisha vizuri tu. Alikaa pale nyumbani kama wiki mbili hivi, lakini kuna mambo ambayo nilikua siyaelewi elewi, yule kijana alikua na mambo ya kike kike, alikua na tabia za kingie chumbani kwengu na kuongea na mimi kama shoga yake, nilimuambia mume wangu akaniambia kuwa nimuache tu ni utoto.

Siku moja nilikua chumbani kwake, ni chumba cha wagani alichokua akilala, kuna vitu nilikua nachukua katika kabati nikakutana na nguo za yule kijana, kulikua na chupi nyingi za kike. Nilikasirika nikamuita na kumuuliza, mwanzo aliongea kwa kujiuma uma lakini baadaye aliniambia kuwa yeye ni shoga na mume wangu ndiyo kamleta pale akimuambia anakuja kufanya kazi lakini hajui kazi gani ila anamlipa. Nilimuuliza kama wana mahusiano na mume wangu alikataa katakata, tuligombana sana na siku ileile bila kumshirikisha mume wangu nilimfukuza.

Mume wangu alipokuja alikana kabisa kuwa alijua kama ni shoga bali ni mdogo wake na rafiki yake na alikasirika kwa mimi kumfukuza kwani nilimshalilisha. Mimi sikujali, lakini usiku uleule wakati nafanya mapenzi na mume wangu alijifanya kupotea njia, nilishtuka ndipo alinikandamizia na kuniambia kuwa mimi nina mimba hivyo hafurahii kufanya mapenzi na mimi sehemu za kawaida anataka kufanya kinyume na maumbile. Nilikasir8ika sana lakini sikua na nguvu, alinipiga sana siku hiyo, kila nilipojaribu kujitoa alikua ananipiga na alinifanyia mapenzi kinyume na maumbile mpaka alipochoka.

Asubuhi mume wangu aliamka akiwa analia, alilia sana na kuniomba msamaha, alikua akiniambia ni shetani kampitia na hajui kwanini alifanya hivyo, alilia na kuomba nisiondoke kwania tajirekebisha. Alionekana kujutia kuliko siku nyingine yeyote ile. Kwa kawaida mume wangu akifanya kosa si mtu wa kuomba msamaha na kama ukimuuliza uliza sana au ukijifanya kukasirika basi unsishia kupigwa na uumizwa, lakini siku hiyo aliomba msamaha huku akilia kama mtoto, nilishangaa sana na sikua na namna zaidi ya kumsamehe.

Maisha yaliendelea, alibadilika kwa siku tano hivi kisha akataka tenja ule mchezo, aliniambia kashaupenda hivyo nimruhusu, mimi nilikataa, kila nilipokua nikikataa alikua akinipiga, alikua akanipiga sana mpaka kufikia hatua ya kuzimia na asubuhi anaomba msamaha. Hayo ndiyo yalikua maisha yangu, baada ya kuwa namnyima kufanya mapenzi kinyume na maumbile alikataa kabis akufanya mapenzi na mimi na kuanza kubadilisha wanwake kama nguo, alikua akifanya hivyo huku akihakikisha kuwa najua na naumia, kama nikimfumania nisipoongea basi niliambulia kipigo.

Alikua akinipiga kuwa nitakua na mwanaume mwingine ndiyo maana simuonei wivu. Hali ile ilinichosha, niliona kama vile atakuja kuniua. Siku moja nakumbuka ilikua siku ya jumapili, niliamua kuondoka, nilimpigia simu mdogo wangu wa kiume amabye alikua kamaliza chuo na kumuambia kuwa anitafutie chumba kwani kuna rafiki yangu anahitaji chumba cha kupanga. Mdogo wangu alikua hafahamu sana matatizo, hivyo alipopata chumba alinipigia na aliponikosa kwenye simu alimoigia mume wangu na kumuambia kuwa aniambie kune chumba amepata sehemu.

Mume wangu hakujua kuwa nataka kuondoka, alikua safarini Morogoro lakinia liposikia hivyo alipanda gari na kurudi siku hiyo hiyo. Alifika nyumbani na kunikuta nipo tu nasubiria jibu la mdogo wangu, sikutegemea kama anaweza kupata chumba kwa hataka namna ile. Mume wangu alisubiri mpaka usiku ndipo aliniuliza kwanini natafuta chumba, sikumuelewa, nilijifanya sijui chochote, hapo ndipo alianza kunipiga na kuniambia kuwa anhtaaka kumdhalilisha tena kama awali.

“Mimi ni mwanaume, sina kasoro yoyote huwezi kabisa kuniacha, mimi siachwi bali ndiyo naacha!” Alifoka sana huiku akinipiga, alinipiga sana, hakuishia kunipiga kwa ngumi na mateke tu, alinipiga kwa kila kitu kilichokua mbele yake, nilipiga kelele yule Mama akaja kugonga mlango lakini alikua kafunga kwa ndani, aligonga sana lakini haikusiadia, pon a yangu ilikua pale alipoita watu wakaja kuvunja mlango, walinichukua mpaka hospitalini na mume wangu kukamatwa na Polisi. Nilikua nimeumizwa sana, ngeu kila sehemu, mwili umevimba, mimba ilishakua kubwa.

Nilikaa hospitalini kwa siku mbili nikaambiwa mtoto kafia tumboni tena kwa mara ya pili. Alitolewa kwa njia ya upasuaji lakini wakati wakinipasua niliambiwa kuwa kizazi changu kimeharibika sana hivyo kinahitaji kutolewa ili kuokoa maisha yangu. Nilikua katika maumivu makali, sikua na namna zaidi ya kukubaliana nao. Nilijikuta ndani ya siku moja napoteza mtotop pamoja na uwezo wa kupata mtoto mwingine. Nililia sana huku kila mtu akinipa moyo na kuniambia kuwa nishukuru Mungu angalau kashanijalia watoto wawili hivyo sina haja ya kusononeka sana.

Mume wake yuko Polisi, kashapoteza kizazi hivi unafikiri kama atarudi? Je mfano akirudi watakua na amani? Vipi mume wake atajifunza na kubadilika? Lakini vipi asiporudi unadhani maisha yake yatakuaje? Nisikuchoshe fuatilia ukurasa wangu wa 

Post a Comment

Previous Post Next Post