TAFADHALI MAMA USIWAUE WATOTO WANGU 25---26-----+27


Usiku mzima akiwa mahabusu Nancy hakupata hata lepe la usingizi akiwaza idadi kubwa ya mambo lakini kubwa zaidi lilikuwa juu ya mama yake aliyekuwa gerezani Segerea, miaka mitano ilikuwa mingi sana kuvumilia hadi mama yake amalize kifungo na kuungana naye.
Hakuelewa angeishi vipi mpaka atakapoungana na mama yake tena! Alipofikiria kurudi Mwanza alishindwa aliamini hakuwa na ndugu zaidi ya mama pekee baada ya kaka yake Patrick kufariki dunia.
“Nyie machangudoa hebu njooni huku nje upesi!”Sauti ya askari aliyekuwa akihangaika kufungua mlango wa mabahusu ilisikika, wasichana kama kumi hivi waliokuwa na Nancy mahabusu walinyanyuka na kuanza kutembea kwenda nje ya mahabusu.
“Wewe changu mtoto hutaki kutoka siyo? Tutakuacha ushinde na kulala humo ndani, ohoo shauri yako!”
“Mimi?’ Nancy aliuliza.
“Ndiyo kwani wewe ni nani? Mtoto mdogo umekwishaanza biashara ya kuuza mwili utakufa siku si zako!” Alisema askari huyo.’
Maneno hayo ya askari ndiyo yalimfanya Nancy aelewe maana ya neno changudoa na alianza kuyaelewa maswali aliyoulizwa na Lwina usiku.
“Mimi siyo changudoa baba!”
“Wewe ni nani sasa?”
“Mimi ni……….!” Kabla hajamaliza sentensi yake kibao kizito kilitua katikati ya uso wake na kumfanya Nancy afumbe macho ghafla.
“Nyamaza! Wewe ndiye unajifanya unajua sana kujieleza siyo?”
“Siyo hivyo baba!” Alijibu Nancy wakati akitoka nje kuwafuata wenzake.
“Haya nyote poteeni haraka hapa kituoni na tusiwaone tena mtaa wa Ohio usiku mnasikia?”
“Sawa afande!”
Wasichana wote walivaa nguo fupi zilizoacha sehemu zao muhimu nje! Zilikuwa ni kama chupi lakini bado hawakujali walitembea wakicheka, walionekana kuwa wazoefu wa mahabusu kuliko Nancy! Aliwashangaa kwa sababu katika maisha yake hakuwahi hata siku moja kufikiria mwanamke angeweza kuvaa nguo za kuabisha kiasi hicho.
“Nancy wahi twende mdogo wangu!” Changudoa Lwina alimshika Nancy mkono na kuanza kuondoka nae, alilishangaa sana gauni alilovaa, aligundua alikuwa Nancy mgeni katika kazi hiyo.
“Wewe ni msichana mzuri sana na utakuwa unapata pesa nyingi sana kwa usiku moja, lakini nakushauri usiwe unavaa magauni ya aina hii utafikiri unakwenda kanisani! Lazima uiache biashara wazi! Biashara matangazo mdogo wangu!” Lwina alimwambia Nancy wakitembea kutoka kituo cha cha polisi kati kuelekea kituo cha mabasi, watu wote waliokutana nao njiani waligeuka na kuwashangaa.
Nancy alizidi kulia machozi wakati wote wakitembea, alishindwa kabisa kuelewa ni kitu gani kilikuwa kikitokea katika maisha yake, Lwina alizidi kumbembeleza lakini haikusaidia.
“Nyamaza kulia Nancy, hebu niambie hapa mjini kwa hivi sasa hasa unaishi wapi?”
“Mimi?’
“Ndiyo!”
“Mimi ni mgeni!”
“Aisee! Kwa hiyo umekuja kujaribu soko la Bongo siyo? Poa, kwa umri wako soko ni kali na utapata pesa nyingi sana si unajua siku hizi wanaume wanapenda wasichana wadogo wadogo kama wewe ambao bado zimesimama!”
Nancy alimwangalia Lwina kwa mshangao mkubwa! Aligundua ni kwa kiasi gani alikuwa amechanganya mambo lakini hakutaka kumwonyesha waziwazi kuwa alichukizwa sana na maongezi ya kimalaya aliyoyatoa, aliamua kuwa mvumilivu aone mwisho wa jambo hilo.
“Sasa ukitoka hapa unakwenda wapi mdogo wangu?’”
“Sina pa kwenda!”
“Basi twende ghettoni kwetu!”
“Ghetto? Ndiyo mtaa gani?”
“Siyo mtaa ni mahali tunapoishi sisi!”
“Wapi huko?”
“Kinondoni tumepanga chumba na tupo wasichana kama kumi na tano hivi, tunachangia gharama za pango ni mahali pazuri tu!”
Alipofikiria wasichana kumi na tano kuishi chumba kimoja ilimuogofya ndipo alipowafikiria sana watu waliomsaidia segerea, mama Teddy na mumewe lakini alishindwa angewapata vipi, hatimaye aliamua kufuatana na Lwina kwenda Kinondoni! Njaa ilimuuma sana mpaka wakati huo alikuwa hajala kitu chochote tangu aliponunuliwa chakula na mama Teddy na mumewe.
Lwina alikuwa changudoa mzoefu, aliianza kazi hiyo akiwa na umri wa miaka kumi na sita na mpaka wakati huo akiwa na umri wa miaka thelathini alikuwa bado akiendelea kufanya biashara hiyo.
Aliingia jijini Dar es salaam akitokea nyumbani kwao Tanga kama mtumishi wa ndani katika nyumba ya mama mmoja eneo la Upanga, lakini baadaye aliacha kazi hiyo na kujiingiza katika kazi ya ukahaba baada ya kushawishiwa na marafiki zake.
Alikuwa mtoto mdogo mno wakati anaanza na mwanaume wengi walimkimbilia ili kukidhi haja zao kimapenzi na watoto wadogo! Lakini alipofikisha umri wa miaka ishirini na tano kazini, wanaume walianza kumkwepa sababu ya kuchuja kufuatia mkorogo aliopaka usoni kwake ambao ulimbabua ngozi na kumfanya awe na mabaka mengi!
Kwa sababu hiyo akawa anakesha mtaani hadi saa kumi na mbili asubuhi bila kupata hata mwanaume mmoja wa kumlipa shilingi mia mbili! Hali hiyo ilipojitokeza Kazi yake ikawa ni kuwatafutia wasichana wenzake wanaume wa kizungu na kulipwa ujira mdogo!
Alipomwona Nancy kwa mara ya kwanza, kwa uzuri wa sura na ngozi pamoja na umri mdogo aliokuwa nao, Lwina alijua hiyo ilikuwa ni biashara nyingine kwake! Alijua ni yeye ndiye angemmiliki kumuuza kwa mwanaume yeyote aliyemtaka bila Nancy kulifahamu jambo hilo.
“Karibu nyumbani kwetu wala usiwe na shaka utakaa, kula na kulala bila matatizo yoyote nitakusaidia kwa kila jambo hapa mjini mdogo wangu!”“Sawa dada lakini kabla ya yote acha nikusimulie matatizo yaliyonipata, nimeteseka sana hapa duniani na hivi sasa ninavyoongea na wewe mama yangu yupo gerezani amefungwa miaka mitano! Sina mahali pa kwenda na ninahisi sina ndugu!” Aliongea Nancy machozi yakimtoka.
Lwina alionyesha kuwa simanzi kubwa kwa maelezo aliyopewa kiasi kwamba Nancy alipolia naye alichukua kitambaa chake na kujifuta machozi! Nancy akajua alikuwa amekutana na mtu mwema ambaye angemsaidia.
“Hivyo ndiyo dunia ilivyo, pole sana mdogo wangu lakini usiwe na wasiwasi tutasaidiana kwa kila kitu hapa mjini!”
“Dada Lwina twende kwanza unipekea kwenye ile hoteli kubwa ya ......ya....ya...nanihii!”
“Hoteli gani bwana?”
“Ile ya jana pale waliponitupa!”
“Kufanya nini?”
“Kuna kaka yangu yuko pale!”
“Bwanaeee! Twende kwanza homu! Huko hotelini tutakwenda baadaye”
“Tutakuta ameshaondoka!”
Lwina hakujali alizidi kutembea kwenda kituoni, kwa sababu Nancy alikuwa mgeni asingeweza kufika hoteli ya Sheraton peke yake ilibidi aendelee kumfuata Lwina nyuma.
**************
Walipofika ghetto Nancy alishangaa, kilikuwa ni chumba kidogo sana lakini wasichana wasiopungua kumi na tano walilala sakafuni, kila mmoja akiwa ametandika khanga yake! Moshi wa sigara na bangi ulijaa kila mahali chumbani! Karibu kila msichana alikuwa na msokoto au sigara mkononi. Wasichana waliimba na kusema maneno mengi ya matusi, Nancy aliogopa na moyo wake ulianza kwenda mbio alihisi jambo baya lingemtokea ndani ya chumba hicho.
“Usihofu shoga wewe ingia tu hawa ni wenzetu tunafanya nao kazi moja na tunashirikiana katika maisha yetu ya hapa mjini!”
Nancy alisogea kwa unyonge hadi ndani ya chumba, wasichana wote waligeuka na kumwangalia kwa macho ya chuki hawakuonyesha kufurahishwa na ujio wake hata kidogo! Hakuna aliyemkaribisha ndani lakini Lwina alielewa ni kwanini wasichana ndani ya chumba walionyesha kumchukia Nancy, uzuri wake uliwatisha na walijua soko lao lingepungua, mmoja wao alisimama na kumfuata Lwina.
“Duh! Shoga ndiyo nini kutuletea kipingamizi?”
“Msiwe na hofu huyu atakuwa hajipangi Ohio, nitampeleka masaki!”
“Huko huko Masaki shoga, Ohio asitie mguu kabisa tutamuua!” alisema msichana huyo na kusonya kisha akarudi mahali pake.
Maongezi hayo yalizidi kumtia hofu Nancy, mwili wake ulitetemeka kwa hofu, baadaye alikaa katika moja ya kona ya chumba hicho na kuanza kulia machozi, akiwa hapo alishuhudia baadhi ya wasichana wakibadilishana mabomba ya sindano na kujichoma katika mikono yao kisha kulala usingizi pale pale na wengine walichoma unga kwa moto na kunusa nao pia walilala sakafuni! Ingawa Nancy alikuwa mgeni jijini alihisi kilichotumika kilikuwa ni madawa ya kulevya!
“Dada Lwina nataka kuondoka!” Alisema Nancy
“Kwanini?”
“Naogopa wenzako!”
“Kwanini?”
“Watanilazimisha kuvuta madawa!”
“Hawawezi mimi nipo na wananiogopa sana hawa, mimi ndiye niliyewakaribisha katika chumba hiki, ninauwezo wa kuwatimua wote ukabaki wewe!” Lwina alinong’ona kwa sauti ya chini.
Moyo wa Nancy baada ya maneno hayo ya Lwina ulitulia, hofu yake ikapungua, lakini bado mambo yaliyoendelea ndani ya chumba hicho yalimtisha baadhi ya wasichana walipigana na wengine walitukana matusi mazito! Katika maisha yake yote hakuwahi kufikiri wasichana wangeweza kuishi maisha hayo.
Baadaye sababu ya kutokulala akiwa mahabusu Nancy alipitiwa na usingizi na kuzinduka saa kumi na mbili jioni, akiwa amechoka na njaa ikimuuma kupita kiasi, aliyemwamsha usingizini alikuwa ni Lwina.
“Shoga amka ule chakula si ulisema una njaa!” Lwina alimkaribisha Nancy!
“Ahsante dada!” Nancy alijibu akikaa kitako sakafuni na kuanza kujisogeza mahali ulipokuwa mduara na wasichana walioishi ndani ya chumba hicho wakila chakula!
“Huyu ale kwani amechanga?” Aliuliza msichana mmoja ambaye afya yake ilionekana ni mbovu kuliko wenzake wote.
“Jamani mwacheni ale, achange kitu gani na mtu kaja leo hata kazi hajaanza?” Lwina aliwaambia wasichana wenzake.
“Ale leo tu kesho hakuna msosi hapa! Asiyefanya kazi na asile!”
Nancy aliketi katikati ya wasichana wawili ndani ya mduara huo na kuanza kula, chakula kilikuwa kidogo hivyo hakushiba ni kama aliichokoza tu njaa yake na Baada ya chakula hicho wasichana wote walianza kuoga na kuvaa vinguo vyao vifupi na kupaka vipondozi usoni kisha kila mmoja alichukua kimkoba chake na kuchomoka kwenda ambako Nancy hakupafahamu, wakabaki yeye na Lwina peke yao chumbani.
“Wanakwenda wapi?”
“Viwanja!”
“Viwanja gani?”
“Kutafuta mabuzi na wewe jiandae tuondoke!”
“Kufanya nini huko viwanja?”“Hujaelewa tu Nancy?Mbona tangu jana nilikueleza jinsi tunavyoishi hapa mjini! Utafanya kazi gani kama tu una elimu ya darasa la saba kama si kuuza mwili!”
“Kuuza nini?’
“Mwili!”
“Mwili gani?”
“Ngono!”
“Ha!Ha!Ha!Ha!Ha! Hivi hiyo ndiyo biashara mnayofanya? Mimi siwezi kufanya kitu kama hicho hata siku moja!Kwanza sijawahi kukutana na mwanaume kimwili katika maisha yangu mimi bado bikra nitawezaje kufanya jambo hilo?”
“Mama yangu!Wewe bado bikra?”
“Ndiyo!”
“Ndiyo vizuri sasa utalipwa pesa nzuri sana, kuna babu mmoja wa kizungu anatafuta mtoto bikra kwa pesa yoyote ile, shoga vaa nikupeleke ukatengeneze dola!”
“Haiwezekani!”
“Niniii?”
“Sitaki kufanya hivyo!”
“Utaishije hapa mjini sasa? Nani atakulisha? Wewe mjinga nini sisi tukajidhalilishe halafu wewe ule bure? Ah wapi hapo umenoa shoga yangu, jiandae kuendelea na safari yako uendako!” Alisema Lwina huku akimalizia kuvaa kinguo chake kifupi kilichoyaacha mapaja yake yote nje na kuondoka zake huku akisonya na kufunga mlango nyuma yake.
“Hata kama itatokea shida gani siwezi kufanya umalaya mimi!”Masaa mawili baada ya Lwina kuondoka Nancy alipitiwa na usingizi na kulala fofofo lakini alishtuka baada ya majira ya saa tisa na nusu hivi usiku, kilichomwamsha ni muungurumo wa gari uliosikika nje ya nyumba, aliponyanyuka na kukaa, alisikia minong’ono ya watu nje, moyo wake ukashtuka alishindwa kuelewa ni kitu gani kiliendelea nje alihisi kulikuwa na tatizo kwani kama lingekuwa jambo la kawaida watu hao wasingenong’ona.
Ghafla alishtuka mlango ukigongwa aliposikiliza vizuri sauti ya mtu aliyebisha hodi aliitambua, alikuwa ni Lwina.
“Shoga umelala nifungulie basi, nimerudi kulala biashara sio nzuri tafadhali fungua!” Lwina alisema.
Nancy aliposikia sauti ya Lwina bila kusita alinyanyuka na kutembea hadi mlangoni na kufungua mlango, lakini badala ya kuingia Lwina waliingia wanaume watatu wazungu wenye misuli mwili mzima, Nancy alishangaa ni kitu gani kilikuwa kikiendelea, watu wale walimkamata na kumbeba hadi nje huku akilia na kupiga kelele, Lwina alichukua kitambaa na kumfunika mdomoni ili sauti yake isitoke.
Walimpeleka ndani ya gari na wote wakapanda kulikuwa na wanaume wawili zaidi ndani ya gari jumla walikuwemo wanaume watano na Lwina wa sita! sehemu ya nyuma ya gari alikuwepo mbwa mkubwa sawasawa na mbwa wa polisi ! Gari liliondoka kwa kasi ya ajabu kwenda mahali ambako Nancy hakupafahamu, njia nzima alilia akimlaumu Lwina.
“Lwina umejifanya kunisidia kumbe ulikuwa na mpango wa kuniua? Sawa tu Mungu anajua!”
“Siyo hivyo Nancy hawaendi kukua!”
“Sasa wanakwenda kunifanya nini?”
“Kuku………….!” Lwina alishindwa kulimalizia neno la mwisho la sentensi yake.
Je nini kitaendelea?
Nini kitatokea kati ya Patrick na mwinjilisti?


HADITHI: TAFADHALI MAMA USIWAUE WATOTO WANGU 26
MTUNZI: ERIC JAMES SHIGONGO
Hakuwepo mtu asiyemfahamu mzee Willim Smith katika jiji la London alikuwa tajiri aliyemiliki mahoteli makubwa ya kitalii, alikuwa na hisa katika viwanda vingi nchini Uingereza na hata Marekani! Katika umri wa miaka sabini na tano alikadiriwa kuwa na utajiri usiopungua paundi za Kiingereza Bilioni tano, kwa hakika mzee huyu alikuwa shefa.
Hakuwa na familia zaidi ya mtoto wake mmoja wa kiume, huyu aliitwa Keneddy alikuwa na umri usiopungua miaka 10! Mke wake alifariki muda mfupi tu baada ya Keneddy kuzaliwa na baada ya kifo cha mkewe aliyeishi naye kwa muda mrefu bila kupata mtoto na alimpenda kwa dhati,mzee Smith alipatwa na simanzi akashindwa hata kufanya kazi zake mwenyewe!
Alijaribu kuoa mwanamke mwingine aliyeitwa Maria ili aitulize roho yake lakini hakupata alichokitaka,mwaka mmoja baaadye akamuoa mwanamke aliyeitwa Barbara lakini alilazimika kumwacha kwa madai hakupika chakula kizuri kama marehemu mke wake Suzanne, akamuoa Regina aliyekuwa na asili ya Sweden huyu alikuwa mwanamke mzuri kupita kiasi lakini pia alimwacha miezi mitatu baadaye kwa madai hakuwa mcheshi kama marehemu mke wake.
Akamuoa Adriana yeye hakukaa nae hata mwezi mmoja, alimwacha sababu alishindwa kumtunza vizuri mtoto wake Kennedy! Mzee Smith aliendelea kuoa wanawake na kuacha hadi akafikisha idadi ya wanawake saba! Wa mwisho kumuoa alikuwa Geogina huyu aliwahi kuwa mrembo wa Uingereza lakini pia alimwacha kwa sababu hakumliwaza kitandani kama alivyofanya marehemu mke wake.
Tajiri Smith alishindwa kupata mke mwenye sifa kama za marehemu mke wake, alianza kuhisi labda alikuwa na tatizo la kisaikolojia na kuamua kumfuata mtaalam wa magonjwa ya akili, Dr Keen ambaye alimwambia neno moja kuwa ‘everything has its own viscosity” Akimaanisha kila kitu kilikuwa na uzito wake.
Daktari alimwambia mzee Smith kuwa kamwe asingepata mwanamke kama mke wake katika maisha yake kwani binadamu wote wasingeweza kufanana!
Jibu hilo la daktari lilimsononesha na kumtia simanzi tajiri Smith ambaye siku zote alitaka aoe mwanamke mwenye tabia na sifa kama za marehemu mke wake Suzanne! Wanawake wote aliwahi kuwaoa walifanana kwa sura hata na maumbile ya marehemu mke wake lakini tabia zilikuwa tofauti.
Mwaka 1996 kwa sababu ya jibu alilopewa na daktari Smith aliamua kutooa kabisa maishani mwake, kufuatia uamuzi huo aliuza nyumba zake zote katika jiji la London na kununua hisa zaidi katika makampuni makubwa likiwemo shirika la ndege la Uingereza, British Airways kampuni ya mafuta ya British Petroleum na kampuni kubwa ya madawa nchini Uingereza, British Pharmauceutical
s.
Smith alichukua uamuzi huo kwa sababu hakutaka kufanya biashara tena maishani mwake, alitaka kuizunguka dunia akifaidi maisha katika siku zake za uhai zilizobaki, alijua hakuwa na maisha marefu duniani.
Alimpeleka mtoto wake Kennedy katika shule ya kimataifa ya St. Augustine jijini London, ilikuwa ni shule nzuri iliyotumiwa na watoto wa matajiri na viongozi mbalimbali nchini Uingereza, alilipa kila kitu ili mtoto wake akae katika shule hiyo siku zote na yeye alianza safari yake kuzunguka dunia akila raha.
Alianzia Marekani, Australia, India, Indonesia, Afrika ya Kusini, Kenya na hatimaye kujikuta nchini Tanzania katika jiji la Dar es Salaam, kila alikokwenda alisafiri na vijana watano waliokuwa mabaharia katika meli yake ndogo ya kifahari iliyoitwa Queen.
Karibu katika kila nchi alipokwenda alikaa zaidi ya miezi mitatu akila raha kabla hajasonga mbele kwenda nchi nyingine, katika nchi zote alizopita alifanya kila aina ya starehe ikiwemo kufanya uzizi na watoto wadogo wenye umri kati ya miaka hadi kumi kumi na sita, aliitumia hiyo kama njia ya kujistarehesha na kujisahaulisha huzuni ya kuondokewa na mke wake! Aliwanunua watoto wadogo na kufanya nao mapenzi kwa malipo makubwa lakini bado hiyo haikusahaulisha marehemu mke wake.
Kwa sababu ya uzee na unene wa mwili wake mzee Smith alipoteza nguvu zake za kiume taratibu akawa hapendi kabisa kufanya tendo la ndoa wakati mwingine akawa anafurahia kuwaangalia watu wakijamiiana! Hiyo nayo kwake ilikuwa starehe na wasichana walioshindwa kufanya alivyotaka aliwaua usiku huohuo na kuwafukia katika shimo lililokuwa nyuma ya nyumba shirika la Utalii aliyopanga! Wasichana karibu kumi walishauawa kwa utaratibu huo huo.
Aliwaamuru vijana aliosafiri nao kufanya mapenzi na wasichana aliowaleta chumbani kwake na yeye alikaa pembeni akiwaangalia na kuchekelea mzee Smith alifurahia sana kitendo hicho na aliwalipa vijana wake pesa nyingi kwa kazi hiyo.
*******************
Gari lilizidi kukata mbuga likipita katikati ya miti kuelekea sehemu yenye giza nene! Nancy akiwa nyuma ya gari mwili wake ukizidi kutetemeka, hakujua alikuwa akipelekwa gizani kufanya kitu gani! Alihisi labda watu wale walikuwa wakienda kumchuna ngozi yake ama kumnyonya damu biashara iliyokuwa imevuma sana wakati huo jijini Dar es Salaam! Aliendelea kulia akimwangalia Lwina kwa macho ya hasira.
“Lwina kweli umeamua kunisaliti?Kwanini hukuniacha nikaenda zangu badala ya kunileta huku?Kwa nini mniue lakini? Nimewakosea kitu gani jamani?”
“Hawaendi kukua wanaenda kuku…..!”
“Kunifanya nini? Au kunifanyia vibaya na mbwa?”
“Siyo hivyo!” Lwina aliongea huku akitabasamu, wazungu walionekana kutosikiliza maongezi yao.
“Lwina ni heri kuniua kuliko kunifanyia unyama huo na mbwa! Nimekwishakueleza kuwa katika maisha yangu hata huyo mwanaume mmoja tu bado hajanigusa leo iwe ni mbwa au wanaume wengi pamoja? Haiwezekani kwa kweli mtaniua bure sitakubali!”
“What is she saying?”Mzungu mmoja aligeuka na kuuliza .
“She is not ready for sex!” (Hayupo tayari kufanya tendo la ndoa)
“Why?”(kwanini ?)
“She is claiming to be a virgin!”(Anadai eti ni bikira!) Alijibu Lwina huku akisonya.
“She is a big liar! How can she the a virgin at that age? She has to find some one else to lie!”(Ni muongo mkubwa katika umri huo kweli awe bikra? Atafute mtu mwingine wa kumdanganya!) Mzungu mwingine aliitikia na safari iliizidi kusonga mbele wakipita chini ya miti.
Nancy aliyasikia maongezi yao yote ni hapo ndipo alipogundua kazi aliyokuwa akienda kuifanya, kumbe alikuwa amechukuliwa kwenda kufanya mapenzi kwa nguvu.
“Yaani wanakwenda kunibaka kweli?Lwina kwanini umenifanyia hivi lakini? Msaada wako mbona unakuwa wa gharama kubwa kiasi hiki?” Aliuliza Nancy huku akilia kumbukumbu zake zilimrudisha.
“Usijali mdogo wangu hawatakuumiza na isitoshe watakulipa pesa nzuri tu shida zako zote zitakwisha!”
“Sitaki pesa mimiiii, nani amekuambia nataka kuuza uhai wangu sababu ya pesa? Sitaki kufa kwa Ukimwi, sitaki kuwa malaya wewe endelea na kazi yako lakini sio mimi! Alijibu Nancy huku akilia”
Wakati akimalizia sentensi hiyo gari lilisimama mbele ya lango kubwa jeusi, honi ilipigwa na sekunde kama tatu hivi lango lilifunguliwa gari likaingia ndani ambako liliegeshwa vizuri kando ya nyumba nzuri.
Ilikuwa ni nyumba ya kifahari na Nancy aliteremshwa garini na kubebwa akaingizwa ndani ya nyumba hiyo, alipitishwa sebuleni na kupelekwa moja kwa moja hadi ndani ya chumba kimoja kilichokuwa na kitanda kipana, taa kali zilimulika ndani ya chumba hicho na kufanya hali iwe kama mchana.
“Go and call the old man! Today we have a sweet meat to eat!” (Nenda kamwite babu maana leo tuna nyama tamu sana ya kula) Alisema mmoja wao ambaye tayari alishaanza kufungua zipu ya suruali yake.
Tangu mzee Smith aanze shughuli ya kuwatumia vijana hao kumstarehesha kwa kufanya mapenzi na wanawake mbele yake, walikuwa hawajawahi kupata msichana mzuri kama aliyekuwa mbele yao! Waliona dakika haziendi kila mmoja wao alitaka awe wa kwanza walishindwa kuwa wavumilivu.
“Today you made the right choice!”(Leo umefanya chaguo zuri sana!) Alisema mzungu mmoja aliyejaza misuli mwili mzima kama mwana mieleka huku akimgusa Lwina begani.
“She is a newcomer to the city!”(Ni mgeni hapa jijini!)
“Sure?”(Hakika?)
“Yeah!”
Dakika kama mbili hivi baada ya mwenzao kuondoka mlango wa upande wa pili wa chumba ulifunguliwa akaingia mzee mwenye umri usiopungua miaka sabini hivi mwenye ndevu nyingi nyeupe! Alikaa kwenye kiti na kuanza kumwangalia Nancy kwa jicho la tamaa! Kisha akatupa mkono wake hewani kama ishara kuwa vijana wake waanze kazi!
Baada ya ishara hiyo Nancy alitupwa sakafuni na kulazwa chali, nguo zake zote zikachanwa akabaki kama alivyozaliwa! Wanaume wawili walimshika mikono na wengine wawili walimshika miguu na kumsambaza sakafuni! Mwanaume mmoja alivua nguo zake zote na kupiga magoti mbele ya Nancy aliyekuwa akilia kuwaomba wasimfanyie kitendo walichotaka kufanya.
“Please!Please!Please don’t do that on me I have never done it before, I’m virgin yet”(Tafadhali! Msinifanyie hivyo sijawahi kufanya tendo hilo hata mara moja mimi bado bikra)
“Whaaaaat?”(Nini?) Aliuliza kwa mshangao mzungu aliyekuwa amevua nguo zake.
“Do it quickly we have no time to waste!”(Fanyeni haraka hatuna muda wa kupoteza hapa) Alifoka mzee Smith na mzungu aliyevua akaanza kumuangukia Nancy kifuani.
“Eee mungu nisaidie!” Nancy alijikuta akitamka maneno hayo katika hali ya kukata tamaa alijua kazi iliyokuwa mbele yake ilikuwa nzito mno hakuwa na uhakika angeimaliza salama.
“Mwite bwana wakati wa shida zenu nae atakuitika!” Aliyakumbuka maneno aliyojifunza kwa mchungaji Aaron akiwa mtoto mdogo.
Kabla mzungu aliyevua akijiandaa kumwingilia Nancy kwa nguvu hajafanya lolote mzee Smith alisikika akipiga kelele.
“Hey stop! She is so beautiful this one is for me please get dressed and take her to my room!”(Hey! Ni mzuri sana huyu ni kwa ajili yangu tu, hebu vaeni nguo zenu na mmpeleke haraka chumbani kwangu) Alisema mzee Smith.
“Du!” Vijana wote waliokuwa wamejiandaa kumfanyia Nancy ubaya waliguna, walishajiandaa miili yao kwa mashambulizi kitendo hicho kilikuwa ni kama kunyang’anywa tonge mdomoni, mmoja wao alidondosha machozi ya tamaa.
Kwa amri ya mzee Smith, Nancy alinyanyuliwa sakafuni akiwa uchi na kuongozwa kupelekwa chumbani kabla ya kumfikisha wote walimshikashika mwili wake! Nancy alihisi kudhalilishwa na kuendelea kulia, jasho lilikuwa likimtoka mwili mzima hofu itanda kichwani mwake hakujua nini kingetokea kabla ya asubuhi siku iliyofuata.
Mzee Smith alilipitia mlango mwingine na kwenda hadi chumbani kwake, Nancy alipoingizwa alishangaa kumkuta mzee Smith ameketi kitandani, alimpokea kwa mikono miwili na kuwatimua vijana wengine wote waliondoka kwa manung’uniko.
“Get out of my room today is my turn to enjoy alone ok!”(Ondokeni chumbani kwangu leo ni siku yangu ya kufaidi pekee) Alisemea mzee huyo na kuwafukuza vijana.
Kwa sababu miili yao tayari ilishachemka na hawakuwa na njia yoyote ya kuipoza walilazimika kmkamata Lwina na kumvuta kuelekea katika chumba chao kilichokuwa jirani na chumba cha mzee Smith! Lwina alilia akiomba wamwachie lakini hawakumsikiliza.
Walipomfikisha ndani walimchania nguo zake zote na kumwacha kama walivyomwacha Nancy! Lwina alilia akimwita Nancy amsaidie.
“Nancy mwambie mzee Smith aniokoe wananiua!” Alipiga kelele kwa nguvu.
Nancy alisikia kelele hiyo kutoka chumba kwa mzee Smith alikokuwa kimya akimsimulia mzee huyo kila kitu kilichotokea katika maisha yake! Walifikia katika maongezi hayo baada ya mzee Smith kujaribu kumwigilia Nancy kwa nguvu na kushindwa akagundua kweli Nancy alikuwa bikra! Alishangaa sana na kutaka kudadisi ilikuwaje mpaka awe katika hali hiyo pamoja na kuwa na umri mkubwa.
“Pole sana binti na nitakusaidia! Katika kutembea kwangu kote duniani nikikutana na wanawake sijawahi hata siku moja kukutana na msichana wa umri wako akiwa bikra.
“Ndiyo maana nililia sana vijana wako walipotaka kunibaka!”
“Yalikuwa ni makosa makubwa sana na nisamehe sana Nancy, nakupenda Nancy huwezi kuamini!”
“Wewe ni nani kwanza?”
“Ninaitwa William Smith ni raia wa Uingereza ninatalii Afrika, mengi zaidi nitakueleza siku nyingine leo naomba unikubalie kitu kimoja, sitaki kukugusa kabla hujakubali ombi hilo na kama utakataa nitakuacha uende sitaki kukuharibu.
“Lakini mimi ni mtoto mdogo sana baba!”
“Usiwe na wasiwasi nitaishi na wewe mpaka ukomae na ukikubali tutaondoka wote kurudi Uingereza natarajia kuondoka kesho kutwa!”
“Mama yangu je?”
“Tutakwenda sote gerezani kumtembelea na nitamwomba atupe ruhusa ili tuondoke!”
“Mama atakubali haina shida hata kidogo! Lakini akikataa sitaondoka!” Alijibu Nancy, katika muda mfupi tu tayari alishamzoea mzee Smith.
Walilala mpaka asubuhi bila kufanya kitu chochote, Nancy alishangaa kwani hakutegemea alale na mwanaume na asimguse usiku mzima kama ilivyotokea.
*****************
Siku iliyofuata ilikuwa ni Jumamosi Nancy na mzee Smith waliondoka asubuhi na mapema kwenda gerezani Segerea kuonana na Anne! Ilikuwa ni siku ya pili kwa Nancy kufika gerezani lakini tofauti na siku ya kwanza siku hiyo alikwenda ndani ya gari la kifahari aina ya Landcruiser Vx, walishuka na kuandikisha majina yao getini baada ya kueleza kuwa walitaka kumwona mfungwa aliyeitwa Anne!
Walionyeshwa chumba maalum cha kusubiri na muda mfupi baadaye Anne alitokea lakini kama ilivyokuwa kawaida yake inzi wengi walikuwa nyuma yake!Tatizo lake la hedhi mfululizo lilikuwa bado likiendelea. Alishangaa kumwona Nancy akiwa na mzee wa kizungu walisabahiana na Nancy alimtambulisha Anne kwa Mr Smith na wakasalimiana kiingereza.
Anne alifurahi sana kumwona mwanae tena! Furaha yake ilionekana waziwazi na baada ya salamu na maongezi marefu ya kutambulishana Nancy alielezea lengo la safari yao.
“Wee mtoto huyu mzee utampeleka wapi?”
“Mama nimeamua kukubali kwa sababu anataka kunipeleka Uingereza!”
“Sawa lakini……!”
“Mama niruhusu tu nikatafute maisha, nitarudi kabla kifungo chako hakijaisha ili kukuchukua twende kuishi wote Uingereza kama mambo yakiniendea vizuri.
“Basi mwanangu siwezi kuwa na kipingamizi ili mradi wewe mwenyewe umeamua ila nitakukumbuka sana kwa sababu wewe ndiye mtoto pekee uliyebaki baada ya kaka yako kufariki na bila wewe mimi ni kama yatima.
Maneno hayo ya mama yake yalimtia Nancy simanzi akajikuta akilia machozi, Anne nae alishindwa kujizuia akajikuta akibubujikwa na machozi, wote wawili walikumbatiana na kuanza kulia, kilikuwa ni kipindi kigumu sana kwao!
“Mama ninakupenda sana na ninasikitika kukuacha, lakini sina budi kufanya hivyo maana hapa Dar es Salaam sina hata mahali pa kuishi yaliyonipata jana ni makubwa lakini labda ndiyo ilikuwa njia ya kukutana na mzee huyu!”
“Ahsante mwanangu lakini unamwamini mzee huyu?”
“Sio sana mama najaribu tu litakalokuwepo mbele Mungu analijua!”
“Muda wako wa kukaa hapa umekwisha rudi ndani upesi!” Askari Magereza alisema baada ya kumgusa Anne begani.
“Sawa afande!” Aliitikia Anne na kunyanyuka huku akilia hiyo ndiyo ilikuwa siku ya mwisho kuonana na mwanae na hakujua kama wangeonana tena maishani! Ilimsikitisha sana lakini yote alimwachia Mungu!
“What has your mother said?”(Mama yako kasemaje?)
“She has agreed!”(Amekubali)
“Thanks God!”(Ahsante Mungu) Mr Smith alisema huku meno yake yote yakiwa nje, alionyesha furaha bila kificho.
“Why are you so happy!”
“I love you Nancy it is like we have known each other for years!”(Nakupenda Nancy inaonekana kama tumekuwa pamoja kwa miaka mingi) Alisema mzee Smith lakini ndani ya moyo wake aliwaza kitu tofauti ambacho hata Nancy mwenyewe hakukielewa, hayakuwa mapenzi ya dhati ulikuwa ni mpango wa mauaji ya kikatili.
*********************
Aliyoyashuhudia Patrick usiku wa siku hiyo yalimfanya apungukiwe imani sana na Mwinjilisti Heinz! Aligundua hakuwa mtumishi wa Mungu kama wengi walivyofikiria, Patrick aliamua kuifanya hiyo kama siri ili apate kufahamu undani ya mwinjilisti Heinz! Moyoni mwake aliogopa sana kwa sababu alijua wazi jambo hilo lilikuwa siri kubwa na hakujua matokeo yake yangekuwa nini baada ya mwinjilisti kugundua kuwa siri yake ilikuwa wazi.
Alimshukuru Mungu kwa kumpa uamuzi wa kutowaita wahudumu wa hoteli Mwinjilisti alipoanguka chini baada ya kujidunga madawa, aliuahidi moyo wake kuendelea na safari pamoja na upelelezi wake kwa siri kubwa.
Walipotoka Dar es Salaam walikwenda hadi Mbeya ambako walifanya mkutano mkubwa wa Injili kwa wiki moja! Miujiza mingi ilitokea lakini muujiza mkubwa uliowafanya watu wengi waamini kuwa Mwinjilisti Heinz alikuwa na nguvu za Mungu ni pale watu walipoishiwa nguvu mwilini, kulegea na kusikia raha ya ajabu baada ya kuguswa puani na mkono wa Mwinjilisti Heinz uliokuwa na kitambaa kidogo.
“Lakini kama si mtumishi wa Mungu kwanini anafanya miujiza?” Patrick alijiuliza bila kupata jibu, alichanganyikiwa na uwezo aliokuwa nao mwinjilisti Heinz na aliahidi kuendelea kufanya uchunguzi zaidi.
“Ni lazima nilijue jambo hili lazima kuna kitu Mungu ninayemwabudu mimi hawezi kumtumia mlevi wa madawa ya kulevya katika kazi yake!” Aliwaza Patrick.
Kila baada ya nusu saa katika mkutano huo ilikuwa ni lazima Mwinjilisti Heinz ateremke jukwaani na kwenda kwenye hema dogo alilolitumia kama ofisi yake! Patrick alishindwa kuelewa ni kitu gani kilimshusha jukwaani kila mara na alishuka watu wakiwa wamefumba macho baada ya kuwaamuru wafanye hivyo wakati wakisali.
“Ni lazima nijue! Na Mungu nisaidie!” Aliwaza tena Patrick na kuamua kuzunguka nyuma ya hema alilolitumia mwinjilisti Heinz, kwa kutumia wembe alichana sehemu fulani ya hema ili kuruhusu jicho lake lione ndani baada ya kukamilisha kazi hiyo alikaa nyuma ya hema kumsubiri Mwinjilisti Heinz ashuke jukwaani.
Haikuchukua hata dakika kumi Patrick alimsikia Mwinjilisti Heinz akiwaamuru watu wafumbe macho ili waombe, watu wote waliinamisha nyuso zao chini na Mwinjilisti alikimbia mbio hadi ndani ya hema! Jicho la Patrick lilikuwa kwenye tundu likichungulia ndani aliyoyashuhudia yalimfanya atetemeke mwili mzima.
Baada ya kuingia ndani ya hema Mwinjilisti Heinz alifungua moja ya mabegi yake na kutoa kichupa kidogo kilichokuwa na unga na kuumimina kwenye kiganja chake na kuuvuta puani kama ambavyo Wamasai huvuta ugoro! Kisha akachukua kitambaa alichotumia kuwagusa nacho watu puani na kukimwagia unga huo ndipo akatoka mbio kurejea tena jukwaani.
“Haiwezekani hawezi kuendelea kuharibu watu na madawa kiasi hiki!” Patrick aliwaza akitembea kwenda jukwaani alikuwa ameamua kuitoboa siri.
Je Patrick atatoboa siri hiyo na akitoboa kitatokea nini?
Je, Nancy kapata mkombozi au amefuata mauti yake?



HADITHI: TAFADHALI MAMA USIWAUE WATOTO WANGU 27
MTUNZI: ERIC JAMES SHIGONGO
Mzee Smith alimwangalia Nancy kwa jicho la mshangao, hakutegemea kukutana na binti mzuri kama huyo katika Afrika tena aliyedai ni bikra.
“Ni mzuri lakini nasikitika atakufa kama wasichana wengine niliowahi kuwaua! Sijui kwanini nachukia wanawake kiais hiki? Mwanamke pekee niliyewahi kumpenda ni Suzanne na alipokufa huyo wanawake wengine wote walikosa thamani!
“Why are you looking at me with such deep penetrating eyes?”(Kwanini unaniangalia kwa macho makali kiasi hicho?) Nancy alimuuliza tajiri Smith.
“Because I love you Nancy and I’m incomplete without you!”(Ni kwa sababu ninakupenda sana Nancy na mimi nikipande bila wewe!) Aliongea mzee Smith akitabasamu lakini tabasamu lake lilikuwa la kinafiki, yote hayo Nancy hakuyatambua.
Mzee Smith alijua siku moja lazima angemuua Nancy hiyo ndiyo ilikuwa kawaida yake, alishaua wanawake wengi baada ya kifo cha mkewe, siku zote katika mahusiano yake na wanawake aliishia kuwaua.
“May be I should leave her alone! I don’t want kill an innocent woman again! I’m tired of killing!”(Labda nimwache aende zake, sitaki kuua mwanamke asiye na hatia tena, nimechoka kuua!) Aliwaza tajiri Smith ambaye moyo wake ulijaa huruma.
Wakati akiendelea kuwaza hayo tayari walishafika maeneo ya Ukonga na ghafla Nancy alipotupa macho yake pembeni alishtuka, alikuwa amemwona mtu aliyemfahamu.
“My sister!”(Dada yangu!) Aliongea kwa sauti mpaka mzee Smith akashtuka.
“Your sister?You haven’t told me you have a sister downtown!”(Dada yako? Lakini hujaniambia una dada hapa mjini)
“Wait!”(Subiri!) Nancy alisema na kuanza kushusha kioo cha dirisha na kuchungulia nje
“Mama Teddiiiiiiiii!” Nancy alipaza sauti na mwanamke aliyekuwa akipita kando kando ya barabara aligeuka na kuangalia nyuma alionekana kushtuliwa na sauti hiyo.
Nancy alimuomba mzee Smith aegeshe gari lake pembeni na alifanya hivyo, akashuka na kuanza kukimbia kumfuata mwanamke aliyekuwa akitembea kulifuata gari lao lililoegeshwa kando ya barabara ielekeayo uwanja wa ndege wa Dar es salaam.
“Ha! Wewe mtoto ulikuwa wapi siku zote hizi?”
“Dada ni marefu ila namshukuru Mungu kunikutanisha tena na wewe kwani nilishakata tamaa kabisa ni mengi yaliyonipata lakini namshukuru Mungu amekuwa na mimi!” Alijibu Nancy wakiwa wamekumbatiana na baadaye alimweleza kila kitu kilichotokea tangu waachane mara ya mwisho viwanja vya jangwani.
“Tulikutafuta sana siku hiyo na tumekuwa tukikutafuta bila mafanikio na hili gari ni la nani sasa?”
“La rafiki yangu!”
“Rafiki yako?Umempataje rafiki mzungu Nancy? Binti usije ukajiingiza kwenye ukahaba ni heri uje uishi nyumbani kwetu kama una shida!” Alisema mama Teddy!
“Siyo ukahaba dada ila…!” Nancy alishindwa kumalizia sentensi yake kwani tayari walishafika mahali gari lilipoegeshwa.
“Mr Smith meet my sister Mrs Kidubo, she is nice woman!”(Bwana Smith tafadhali kutana na dada yangu mama Kidubo ni mwanamke mzuri sana) Alisema Nancy akimgusa mzee Smith begani na bila kuchelewa Smith alishuka ndani ya gari lake na kumsalimia mama Teddy wakati Nancy akimtambulisha mama Teddy kwa mzee Smith.
“Meet my husband to be, mr Smith we met in a very miraculous way, we shall be traveling to London soon!(Kutana na atakayekuwa mume wangu, bwana Smith tulikutana naye kimiujiza na tutasafiri pamoja kwenda London hivi karibuni)
Mama Teddy alibaki mdomo wazi baada ya utambulisho huo, hakuamini maneno aliyoyasikia kutoka kwa Nancy kwani mzee Smith alikuwa mzee mno kumuoa binti huyo.
“Unaniambia ukweli Nancy?”
“Ndiyo dada hivi unavyotuona tumetoka gerezani kumuaga mama!””Aisee siamini hata kidogo!”
“Kwanini huamini dada?”
“Mambo yamekwenda harakaharaka mno lakini unamfahamu vizuri huyu mzungu?”
“Siwezi kusema namfahamu sana ila yote nimemwachia Mungu!”
Waliendelea kuongea mengi pembeni wakiamini mzee Smith hakusikia kiswahili na hivyo ndivyo ilivyokuwa. Baadaye waliagana Nancy akachukua anuani ya mama Teddy na alimpa jina la mama yake ili amtembelee gerezani mara kwa mara.
“Ninaamini nikiwa London nitapata taarifa za mama kutoka kwako au siyo? Nitakupigia simu mara kwa mara!”
“Haina tatizo hata kidogo nakutakia kila la kheri katika maisha yako Nancy!”
“Msalimie sana mume wako na pia mtoto wenu Teddy mwambie akikua awe na tabia kama yako sawa dada?”
“Ok!” Alijibu mama Teddy na kuendelea kusimama akishuhudia gari lililombeba Nancy likiondoka kueleka mjini.
******************
Maisha ya Nancy yalishaanza kurejewa na matumaini tena baada ya mateso ya muda mrefu alipokutana na mzee Smith! Alimwona mkombozi na alimwamini kwa muda mfupi sana.
“Sitaki kumuua binti huyu!” Alijikuta akitamka maneno hayo bila kujua kuwa Nancy alimsikia.
“Binti gani?”Nancy aliuliza.
“Ah!Ah!Ah! Mh!Mh! Nimetamka tu kwa bahati mbaya!” Alijibu mzee Smith lakini alionyesha wasiwasi mkubwa.
Hiyo ilikuwa ni dalili tosha kabisa kumuonyesha Nancy kuwa mzee aliyekuwa naye alikuwa mtu wa hatari na alifikiria kumfanyia kitu kibaya lakini bado Nancy hakuelewa kitu chochote alizidi kufurahia kila kilichoendelea.
Walipofika kwenye nyumba aliyopanga mzee Smith akiwa nchini Tanzania Nancy alipika chakula na wakala kisha kuingia ndani kulala. Ni usiku huo ndio mzee Smith alipotaka kuujua ukweli kama Nancy alikuwa bikra au la! Alitumia nguvu zake zote na kumwingilia kimwili, hakuyaamini macho na hisia zake alipokuta kitu alichosema Nancy kilikuwa kweli.
“Nancy!”
“Yes!” Aliitikia Nancy huku akilia.
“I cant believe this!You are a virgin! How did you keep it?”(Nancy siwezi kuamini kumbe kweli wewe ni bikra? Umeitunza tunza vipi?)
“You are the first man in my life mr Smith, so please never hurt me!”(Wewe ni mwanaume wa kwanza katika maisha yangu bwana Smith tafadhali nakusihi kamwe usije kuniumiza)
“I will never do anything to hurt you, believe me Nancy!”(Sitafanya kitu chochote kile kukuumiza, niamini Nancy)
Furaha aliyokuwa nayo moyoni mwake mzee Smith ilikuwa si rahisi kuieleza, hakutegemea katika maisha yake kukutana na msichana bikra!Alishazunguka sehemu nyingi duniani akimtafuta msichana wa aina hiyo lakini hakufanikiwa kumpata.
“I have gone around the world looking for a virgin but never got one! People called me a male prostitute simply because I made love to a lot of girls searching for a virgin! I’m happy I have found what I wanted!”(Nimezunguka dunia nzima nikitafuta bikra lakini sikufanikiwa kumpata hata mmoja!Watu wameniita mimi malaya wa kiume kwa sababu nimefanya mapenzi na wasichana wengi sana nikimtafuta bikra! Leo nina furaha nimepata nilichotafuta) Aliongea mzee Smith akionyesha tabasamu.
****************
Nancy hakuamini siku iliyofuata baada ya taratibu zote kukamilika kujikuta akiwa ndani ya ndege ya shirika la British Airways wakisafiri kwenda Uingereza! Machozi yalimtoka wakati ndege hiyo inauacha uwanja wa ndege wa Dar es Salaam, mawazo yake yote yalikuwa kwa mama yake aliyekuwa gerezani, aliumia kumwacha lakini hakuwa na la kufanya na alijipa moyo wa siku moja angerudi kumchukua mama yake wakaishi wote Uingereza.
“Will mom join us in the UK after her sentense?”(Je mama atatufuata Uingereza baada ya kifungo chake?)
“No problem I would love to see your mom staying with us! Because I love you then why hate your mom?”(Hiyo haina tatizo nitafurahi sana kama mama ataishi na sisi siku moja!Kama ninakupenda wewe kwanini nimchukie mama yako?) Aliuliza mzee Smith.
Waliingia uwanja wa ndege wa Heathrow saa moja jioni, giza lilishaanza kutanda kila mahali, Nancy alishangazwa na wingi wa taa zilizowaka angani katika majengo marefu yaliyokuwemo katika jiji la London, ilikuwa ni mara ya kwanza katika maisha ya Nancy kuwa katika jiji kubwa na lenye majengo marefu kiasi hicho, hakuyaamini macho yake. Kuna kipindi alihisi ni ndoto iliyokuwa ikimtokea.
“Welcome to London my wife to be!”(Karibu London mke wangu mtarajiwa) alisema mzee Smith akimpigapiga Nancy mgongoni.
“Thanks!”(Ahsante)
Wote waliteremka katika ndege na kutembea hadi nje ya uwanja nyuma yao wakifuata vijana waliosafiri na mzee Smith! Nancy aliwachukia sana vijana hao na aliona aibu kila alipogonganisha nao macho, walikuta magari yakiwasubiri kila mahali alikopita mzee Smith watu walimpigia saluti kuonyesha heshima kubwa.
Walifunguliwa mlango katika moja ya magari lililoonekana kuwa la kifahari kupita kiasi na kuingia hadi ndani na milango ilifungwa nyuma yao.
“People treat you like a king sir!(Watu wanakuchukulia kama mfalme mzee!)
“Not real!”(Siyo sana)
Magari yaliondoka uwanja wa ndege kuelekea katika nyumba pekee aliyobakiza baada yakuuza kila kitu, nyumba hiyo ilikuwa katika kitongoji cha Southampton, njiani Nancy alizidi kushangazwa na uzuri wa Uingereza! Haikuwachukua muda mrefu sana wakawa wamesimama mbele ya ngome kubwa na lango likafunguliwa magari yote yakaingia ndani, ulikuwa ni msafara wa magari kama kumi na tano hivi yote yakiwa na rangi nyeusi! Mlango wa gari walilopanda ulifunguliwa na wote wakateremka na kusimama nje, mzee Smith alionekana kufurahi muda wote na kabla hawajafanya lolote, alikuja mwanamke mmoja akapiga magoti na kumgusa Nancy miguuni.
“Welcome madamme! We promise to love and respect you!”(Karibu mama tunaahidi kukupenda na kukuheshimu) Alisema mwanamke huyo.
Nancy alishindwa kujibu kitu chochote kwa sababu mama huyo alilingana kabisa na mama yake mzazi kwa umri, kitendo cha kuja kumpigia magoti kilimfanya ajisikie vibaya.
“Thanks!”(Ahsante) hatimaye alijibu na mama huyo alinyanyuka na kuwaongoza kuingia ndani kwa heshima zote.
“Who told them that I was coming here with you?(Nani aliwaeleza kuwa nilikuwa nakuja na wewe?)
“I Phoned them yesterday to make the arrangements, told them that I was coming here with the queen of my family!”(Niliwapigia simu jana kufanya maandalizi na niliwaweleza nilikuwa nakuja na malkia wa familia yangu!)
Walipoingia ndani Nancy alishangazwa na uzuri wa nyumba hiyo kwani kulikuwa na kila kitu ambacho binadamu alihitaji, walifanyiwa kila jambo walilotaka kufanya! Walivulishwa viatu, walikalishwa vitini na kupepewa na vitambaa ili wasitoke jasho! Nancy alizidi kushangaa, kwake hayo yalikuwa ni maajabu ambayo hakuwahi kutegemea yangetokea maishani mwake siku zote alijua angekufa masikini.
“Ningependa zaidi kama mama yangu pamoja na kaka yangu Patrick wangekuwepo kushuhudia mambo haya!”Aliwaza Nancyna kuhuzunika.*****
Wiki moja baada ya kuwasili harusi kubwa ya kifahari ilifanyika watu wote maarufu nchini Uingereza kama wacheza sinema, wanamuziki, walihudhuria! Nancy akawa ameolewa, watu wote waliohudhuria walimshangaa mzee Smith kwa uamuzi wake wa kuoa msichana aliyelingana na mtoto wake wa kiume Kennedy.
Baada ya hapo maisha yaliendelea vizuri, Nancy akaheshimiwa na watu wote kama mke wa tajiri Smith, watu wote katika familia yake walimuogopa na kumtetemekea, kitu cha kwanza alichofanya baada ya ndoa ni kuhakikisha kuwa vijana wote waliomchukua kutoka kwa Lwina kumpeleka kwa mzee Smith wamefukuzwa kazi! Hakuwapenda hata kidogo alifanya hivyo ili kulinda heshima yake.
Je nini kitaendelea?

Post a Comment

Previous Post Next Post