🔞🔞LADYBOY 01 🔞🔞

 (Nafanya yote ili siku moja niwe mwanaume)

Utangulizi..
Jina langu naitwa Alehandro Msosa,kwa sasa ninaishi jijini Dar es salaam.Ni kijana niliyepitia masaibu mengi ambayo ukisimuliwa mengine yanasikitisha, kusismua na kuelimisha.Yote ni kuhusiana na safari yangu ya kutaka kubadili jinsia ama maumbile mchanganyiko ya kike nay a kiume niliyozaliwa nayo.
Baada ya kujuana na kaka mshua master nikaona nishee naye simulizi hii ambayo natumani mtaipokea vizuri tu ingawa ndani yake kuna makwazo mengi na mateno machafu naombeni mnisamehe kwa hilo lakini nia yangu ni kuburudisha na kuelimisha kama ilivyo kauli kuu ya kakamshua baada ya kila tamati ya simulizi.
ANZA..
Nilizaliwa mkoani Mwanza katika wilaya ya Nyamagana yani pale Mwanza mjini.Nililelewa na mama yangu pekee kwani baba yangu alimtelekeza mama punde tu baada ya kumpa ujauzito, hivyo tangu kuzaliwa kwangu sikuwahi kumuona wala kumfahamu baba yangu mzazi.
Pamoja na yote maisha tuliyoishi na mama yalikuwa magumu sana yaliyojaa masimango na kuko 

Post a Comment

Previous Post Next Post